• Breaking News

    ..

    ..

    Tuesday, 6 December 2016

    TANGAZO LA AJlRA YA DHARURA KATlKA SEKTA YA AFYA

    uhuruggggggggggggggggg
    uhurugggggggggggggggggJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
    WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
    Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imepata kibali cha mpango wa Ajira ya dharura kwa wataalamu wa “fani za Tabibu na Wauguzi. Mpango huu utaendeshwa chini ya mradi, kwa ufadhili wa fedha za Mfuko wa CDC, Award No. 5U2GGH001062-03 kwa muda wa miaka miwili.
    Mradi utaajiri watumishi 192 ambao watapangiwa kufanyakazi kwenye halmashauri za wilaya 40 zenye uhaba mkubwa wa watumishi wa kutoa huduma za afya hasa kwa waathirika wenye virusi vya UKIMWI. Watumishi hawa watalipwa mishahara na stahiki nyingine kwa kufuata taratibu na kanuni za serikali. Watumishi wanaotakiwa ni Tabibu Wasaidizi (Clinical Assistant) 95 wenye ngazi ya Astashahada (Certificate in Clinical Medicine) na Wauguzi (Enrolled Nurses) 97 wenye ngazi ya Astashahada (Certificate in Nursing and midwifery).
    Wizara inakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa watanzania wenye sifa zilizotajwa hapo juu, wawe na cheti cha kumaliza kidato cha nne pamoja na cheti cha taaluma aliyosomea kutoka kwenye chuo kinachotambuliwa na serikali. Barua ya maombi ioneshe wilaya ambayo mtumishi atapenda apangiwe kufanyakazi kati ya wilaya zilizopendekezwa hapo chini. Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 14/12/2016.
    Maombi yote yatumwe kwa:-

    Katibu Mkuu
    Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,
    6 Samoral Machel Avenue,
    S.L.P 9083,
    11478, Dar es Salaam.
    Tanzania
    05/12/2016

    Orodha ya Halmashauri za Wilaya na idadi Watumishi waliopendekezwa.
    Na.MkoaHalmashauri  (Wilaya)Tabibu WasaidiziWauguzi WasaidiziJumla
    1Arusha1. Arusha CC336
    2Dar es Salaam2. Ilala MC336
    3. Kinondoni MC336
    4. Temeke MC336
    3Dodoma5. Dodoma MC235
    4Geita6. Geita DC224
    5Iringa7. Mufindi DC336
    8. Iringa MC224
    6Kagera9. Bukoba DC336
    10. Muleba DC224
    7Kigoma11. Kigoma Ujiji MC235
    8Kilimanjaro12. Moshi DC336
    9Lindi13. Lindi MC224
    10Mara14. Musoma MC224
    15. Rorya DC224
    11Mbeya16. Chunya DC224
    17. Kyela DC336
    18. Mbarali DC224
    19. Mbeya CC336
    20. Mbeya DC336
    21. Mbozi DC224
    22. Rungwe DC224
    12Morogoro23. Morogoro MC336
    13Mwanza24. Nyamagana MC336
    25. Sengerema DC224
    14Njombe26. Njombe TC224
    27. Wanging’ombe DC224
    15Rukwa28. Sumbawanga DC224
    29. Sumbawanga MC224
    16Ruvuma30. Mbinga DC224
    31. Songea MC224
    17Shinyanga32. Kahama DC224
    33. Kahama TC336
    34. Shinyanga MC224
    18Tabora35. Igunga DC224
    36. Nzega DC224
    37. Tabora MC336
    19Tanga38. Korogwe TC224
    39. Muheza DC224
    40. Tanga CC336
    Jumla9597192

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI