Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi,
ametangaza kiama kwa wamiliki ardhi ambao hawajalipa kodi ya pango la
ardhi na kutoa muda hadi April 30 mwaka huu kuhakikisha wanalipa kodi
hiyo.
Waziri
Lukuvi ameyasema hayo kwenye ziara mkoani Mwanza alipotembelea
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela na Halmashauri ya jiji la Mwanza na
kuziagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha zoezi hilo la ukusanyaji
wa kodi ya pango la ardhi linakamilika kwa wakati.
Amewataka wakuu wa idara za ardhi nchini kusajili hati za viwanja kwa wanaohitaji ardhi kwa kutumia majina yanayotambulika kwenye vitambulisho vya taifa NIDA ili kuepuka udanganyifu ambapo kodi hiyo ipo kisheria.
Waziri Lukuvi pia amezitaka Halmashauri zote nchini kuhakikisha wanapima maeneo yote yakiwemo mamlaka za viwanja vya ndege, hifadhi za wanyama na misitu taasisi zinazomiliki ardhi na wizara zote kupimwa.
Amewataka wakuu wa idara za ardhi nchini kusajili hati za viwanja kwa wanaohitaji ardhi kwa kutumia majina yanayotambulika kwenye vitambulisho vya taifa NIDA ili kuepuka udanganyifu ambapo kodi hiyo ipo kisheria.
Waziri Lukuvi pia amezitaka Halmashauri zote nchini kuhakikisha wanapima maeneo yote yakiwemo mamlaka za viwanja vya ndege, hifadhi za wanyama na misitu taasisi zinazomiliki ardhi na wizara zote kupimwa.
No comments:
Post a Comment