• Breaking News

    ..

    ..

    Friday 26 January 2018

    Mkuu Wa Shule ya Halisi na Afisa Elimu Kata ya Majohe Nancy Peter Wilaya ya Ilala Watumbuliwa

    Mkuu wa shule ya Sekondari Halisi Jacob Mosha, akiwa katika kikao na Afisa Elimu Mkoa wa Dar es Salaam, ambapo amesimamishwa kazi  kupisha  uchunguzi baada ya kubainika akichangisha wanafunzi michango(Picha na John Luhende) 


    Mkuu wa shule ya Sekondari Halisi, iliyopo Kata ya Majohe Jacob  Mosha, pamoja  Afisa elimu kata ya Majohe Nancy Peter, wamesimamishwa kazi  kwa kosa la kuchangisha michango wanafunzi wa shule hiyo shilingi 2500 ya kitambulisho, na Nembo ya shule shilingi 4000.
    Akizungumza  shuleni hapo, Afisa Elimu wa mkoa wa Dar es Salaam, Hamis Lisu, amesema Mwalimu huyo amesimamishwa ili kupisha uchunguzi.
    Lissu , akiwa  ameambatana na Afisa Elimu Wilaya Elizabeth Ngonyani, na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala,  Palela Msogela, baada ya kuzungumza na walimu na wanafunzi shuleni hapo  wamesema wanapata  vitisho kutoka  kwa Mkuu  huyo kuwa atakaye  sema  atafukuzwa ama kuhamishwa  shule.
    Amesema, kuchangia mchango wanafunzi ni kinyume cha Sheria  waraka namba 3 wa elimu bila malipo  wa  mwaka 2016.
    "Pamoja na kuwepo waraka huu  nimekuta nimewasisitiza  walimu kutowachangisha wanafunzi  kama vile haitoshi  juzi tena baada ya  Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe kulizunguza na kulitilia mkazo nimetuma Barua kwa Wakurugenzi kuwataka wote walikuwa  wamepewa vibali vya kuchangisha waache mara moja  kwakuwa  mkuu wa mkoa alivifuta vyote". Amesema Afisa Elimu.
    Pamoja na hayo amesema ataunda Kamati ikiongozwa na yeye na Mkurugenzi, itaanza kazi ya uchunguzi Juma tatu tarehe 29 January na Mkuu wa shule na Afisa Elimu kata  ili kupisha uchunguzi wa Kamati  na pia amemwaagiza  Mkurugenzi kutafuta mtu wakukaimu nafasi ya Mratibu kata.
    Pia amewataka walimu  ambao wanatishiwa maisha na Mkuu wa shule kubakia shule hapo na atakaye tishiwa  atoe taarifa kwake.

    Hata hivyo Mwalimu huyo amejitetea kuwa amewarudishia fedha zao wanafunzi wote aliwachangisha, na wanafunzi nao wameuthibitishia kurudishiwa fedha zao.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI