Na Stahmili mohamed.
Ikiwa
ni miaka 64 tangu kuanzishwa kwa siku ya ukoma duniani toka mwaka 1954,
Leo Tanzania imeungana na nchi nyingine duniani kuadhimisha siku hiyo
huku kaulimbiu ikiwa ni "tokomeza ulemavu unaotokana na ukoma miongoni
mwa vijana".
Akiongea
na vyombo vya habari Leo makao makuu ya Wizara ya afya kwa niaba ya
waziri mkuu, naibu waziri wa afya Faustine Ndugulile amesema kuwa
katika maadhimisho hayo lengo la kuikumbusha jamii na kuielimisha juu ya
ugonjwa wa ukoma na kuongeza kuwa bado kuna changamoto kubwa kwa baadhi
ya maeneo hapa nchini.
Akitaja
maeneo ambayo bado yana changamoto ya ukoma Ndugulile amesema kuwa kuna
mikoa 10 ambayo inagundua wagonjwa wapya kila mwaka ambayo ni Lindi,
Rukwa, Mtwara, Morogoro, Pwani, Tanga, Geita, Dodoma, Tabora na kigoma.
Lakini
pia amezitaja wilaya 20 ambazo kiwango cha ukoma kipo juu sana na bado
hazijafikia lengo la utokomezaji ambazo ni Liwale, Nkasi, Ruangwa,
Nanyumbu, Shinyanga manispaa, Kilombero, Mafia, Pangani, Mvomero, Masasi
mjini, Lindi vijijini, Kilwa, Mpanda, Nachingwea, Rufiji, Korogwe,
Mkinga, Ulanga, Morogoro vijijini na Chato.
Sambamba
na hayo naibu waziri amezitaja dalili za awali za ugonjwa wa ukoma
ambazo ni kutokwa mabaka kwenye ngozi yenye rangi ya shaba na hayawashi
wala kuuma na pia mabaka haya hukosa hisia ya joto, mguso au maumivu na
kuongeza kuwa dalili nyingine za ukoma ni pamoja na vijinundu kwenye
ngozi hasa usoni au masikioni na uvimbe na maumivu kwenye mifupa ya
fahamu.
Pia
Ndugulile ameeleza mipango ya serikali katika kutokomeza kabisa ugonjwa
huo ambao hutokana na vimelea vya ukoma viitwavyo Myco-Bacteria Leprae
na kusema kuwa serikali imechukua hatua ya kuendesha kampeni ya
ugunduaji wa wagonjwa wapya kwa kila kijiji ndani ya harmashauli
zinazoongoza hapa nchini.
Pia
ameongeza kuwa serikali imejipanga kuendesha zoezi la kutoa kinga
katika ngazi ya kaya sambamba na kuagiza na kusambaza dawa za kutosha za
ukoma nchini kote.
Aidha
naibu waziri amewahasa wagonjwa wote pamoja na jamii inayowazunguka
kujitokeza ili kuweza kupata matibabu yanayostahili na kuachana na mila
potofu huku akisisitiza kuwa ugonjwa wa ukoma siyo ugonjwa wa kurogwa na
kuongeza kuwa matibabu ya ukoma hutolewa bure kabisa katika vituo vyote
vya afya hapa nchini.
Mwisho
kabisa naibu waziri ameiomba jamii kujenga tabia ya kuchunguza miili
yao Mara kwa Mara ili kuweza kuuzuia ugonjwa ukiwa katika hatua ya awali
jambo ambalo litasaidia pia kupunguza kusambaa kwa ugonjwa huo.
No comments:
Post a Comment