..
Tuesday 13 December 2016
Habari
Kampuni ya Grand Tech ya nchini Tanzania imejitolea kujenga barabara ya shimo la udongo kwa kiwango cha zege kwa urefu wa Kilomita moja, ikiwa ni ishara ya kuunga jitihada za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda na Rais John Pombe Magufuli.
Akizungumza Jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Kampuni hiyo inajihusisha na ujenzi wa barabara na makazi Atu Patrick Mwakitwange ameeleza kuwa wameamua kuunga mkono jitihada za serikali kwani eneo hilo la Shimo la Udongo lilitengwa na serikali kwa ajili shughuli za bandari hivyo ujenzi huo utarahisisha shughuli hizo na wataendelea kuunga mkono jitihada za Rais Magufuli.
No comments:
Post a Comment