• Breaking News

    ..

    ..

    Monday 31 July 2017

    BARAZA LA MADIWANI MJI WA KIBAHA LAADHIMIA MKUU WA IDARA YA MAZINGIRA NA MAJI WAWAJIBISHWE

    IMG-20170731-WA0052
    Mbunge wa jimbo la Mji wa Kibaha ,Silvestry Koka akieleza maadhimio ya baraza la mji huo yaliyotolewa kwenye baraza la madiwani
    IMG-20170731-WA0053
    Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kibaha, Lucy Kimoi akizungumza jambo katika baraza la madiwani la Mji huo .(picha na Mwamvua Mwinyi)
    ……………………..
    Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha
    BARAZA la madiwani la halmashauri ya Mji wa Kibaha ,Pwani ,limeadhimia mkuu wa idara ya mazingira Tumaini Kaila na wa idara ya maji Grace Lyimo wachukuliwe hatua na mamlaka za ajira zao endapo watabainika kuzembea kusimama majukumu yao  .
    Akielezea maadhimio ya madiwani hao ,mbunge wa jimbo la Mji wa Kibaha ,Silvestry Koka ,alisema baraza hilo pia limemkataa mkuu huyo wa idara ya mazingira kutokana kukosa ushirikiano na kushindwa kusimamia hali ya usafi ya mji huo ambayo hairidhishi .
    Aidha limeitaka mamlaka husika ya ajira yake imchukulie hatua stahiki kwa mujibu wa ajira yake. 
    Koka alisema wameshindwa kumvumilia mkuu huyo wa idara ya mazingira kwani huwezi kufanyakazi pasipo kuwa na mahusiano mazuri na madiwani wala watendaji wengine .
    “Maeneo mengi na ya wazi hayapo katika usafi hivyo na hili nalo tumeshapiga kelele ,tumeshauri ,hashauriki ,ni bora mamlaka husika imuwajibishe .” alisema Koka .
    Hata hivyo ,madiwani hao wameelekeza wakandarasi washauri na wasimamizi wa miradi ya maji wachukuliwe hatua zile zinazostahiki kwa kushindwa kusimamia miradi hiyo na kusababisha hasara ya mil.132 .
    Walitaka  wakandarasi hao wachukuliwe hatua kwa kulingana na mikataba yao.
    Koka alibainisha kwamba ,waajiriwa wa halmashauri waliosimamia miradi ya maji wakiongozwa na Grace Lyimo ,mamlaka zao zinazowasimamia ziangalie hatua za kuwachukulia endapo watabainika kufanya uzembe .
    Katika hatua nyingine ,mbunge huyo aliishauri halmashauri na watendaji kukamilisha miradi mbalimbali ambayo ni viporo ikiwemo zahanati na majengo ya madarasa .
    Koka alisema miradi hiyo ambayo haijakamilika ikamilishwe kabla ya kuanza mipya  ya aina ile ile .
    Alielezea kuwa ,haina budi fedha zinazoingizwa na serikali ikakamilisha miradi lengwa kwa maslahi ya jamii kuliko kuishia kati huku mwaka wa fedha mwingine inaanzishwa miradi mingine hivyo kusababisha kuwa na mlundika wa miradi ya zamani .
    Wakati huo huo ,Koka alisema kwa mujibu wa sheria 0.03 ya mauzo au huduma kwa viwanda au kampuni hulipia kodi ya mapato kutokana na bidhaa wanazozalisha .
    Alisema licha ya kulipia mapato kisheria lakini inapaswa halmashauri ikaangalia namna ya kukusanya asilimia kiasi ya mapato kwenye viwanda na makampuni yanayozunguka mji huo kwa ajili ya kujiongezea mapato .
    “Kila anaetoa huduma inatakiwa halmashauri imfikie ili inufaike na wadau wake”alisema Koka .
    Nae diwani wa kata ya Tumbi ,Hemed Chanyika alisema kwa kushindwa kupeleka taarifa za kata za maji imechangia kukosa zaidi ya sh mil 100 ambazo wahisani walitakiwa kuchangia kuleta Maji mjini Kibaha .
    Awali akiibua hoja hiyo ya miradi ya maji kusuasua alisema wakandarasi na watendaji husika wa idara hiyo watafutiwe kazi nyingine .
    Chanyika alielezea wananchi wanataka kuona majibu na matokeo ya miradi inayotekelezwa na serikali na wahisani hivyo kama haisimamiwi kikamilifu inakatisha tamaa .
    ” Miradi ya nyuma tumeshapata hasara yenye zaidi ya mil. 132  na kutoletwa taarifa za kata tumekosa mil.100 ambazo tungewezeshwa na wahisani”alisisitiza Chanyika.
    Diwani wa viti maalum mjini humo, Selina Wilson ,alizungumzia changamoto ya kusuasua kwa fedha zinatengwa kwa ajili ya vijana na wanawake .
    Alisema katika halmashauri hiyo fedha hizo hazitolewi zote na zinawekwa kidogo .
    Selina alieleza ,kwa mwaka 2015/2016 kati milioni 306 zilizotengwa lakini zilizopelekwa kwenye vikundi ni milioni 49 pekee,na zilizobaki milioni 256.
    Alisema kwa 2016/2017 zimetengwa milioni 391 zilitolewa hadi sasa ni milioni 174.
    Selina aliomba halmashauri hiyo itupie macho makundi hayo kwa kuyawezesha kupitia fedha zao zote zinazotengwa bila kuyabania .
    Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) Mji wa Kibaha,Maulid Bundala alisema licha ya miradi ya maji kudorora na miradi ya barabara iangaliwe .
    Bundala alisema wakandarasi wa miradi ya miundombinu ya barabara wasimamiwe ili ijengwe kwa viwango vinavyotakiwa na kumalizwa kwa wakati

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI