Hayo yamesemwa na mkurugenzi mkuu wa makumbusho ya Taifa
Bw.Audax Mabula alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana
na onesho hilo ambapo amesema onesho hilo limeandaliwa na makumbusho ya
taifa kushirikiana na mpiga picha Bw.jesper Kirknaes na kudhaminiwa na
ubalozi wa Denmark nchini Tanzania hivyo onesho hilo litafunguliwa rasmi
na Mh.Balozi Einar .H.Jensen kutoka ubalozi wa Denmark nchini Tanzania
tarehe 16 mwezi huu saa 7 mchana eneo la makumbusho hivyo viongozi
mbalimbali wanatarajiwa kuhudhuria.
Hata hivyo Bw.Mabula amesema katika onesho hilo linaitwa
"Karibu Tanzania" ambapo ameeleza kuwa picha mbalimbali zinazohusu
maisha na kazi zilizokuwa zilizokuwa zinafanywa na watu wa enzi hizo
zitatoa mwanga na ufumbuzi wa kifikra kwa kila mmoja kwani zinaonyesha
na kueleza maisha halisi ya watanzania hao waliokuwa mwaka 1968-1977
namna walivyoweza kutengeneza vifaa mbali mbali kama vyungu,majembe na
kila kitu ambacho walichokuwa wanahitaji kwa wakati huo.
Vile vile Bw.Mabula amewataka zaidi vijana kujitokeza
katika onesho hilo kwani watajifunza tamaduni mbalimbali za makabila yao
kwa kuona nyumba halisi za makabila yao,vyombo vyao vya nyumbani kama
chungu,vikapu na kadhalika hivo onesho hilo linaumuhimu zaidi .
Pia Mabula ameongeza kwa kusema kwa wakati huu tuliopo wa
Sera za viwanda tunapata funzo kutoka kwa watanzania wenzete ambao
waliweza kuendesha maisha yao kwa kujitengenezea wenyewe vitu
walivyovihitaji wenyewe hivyo kupitia picha hizo tunaweza kuona
tulipotoka na kujifunza fursa zaidi kwani tunaweza kuviendeleza baadhi
ya viwanda vilivyoachwa na watu hao kwa kujifunza kutengeneza wenyewe
baadhi ya vitu kama majembe na vingine vingi kwani kupitia picha hizo
zinaonyesha hatua kwa hatua walizokuwa wanazifanya watanzania wenzetu.
Naye mpiga picha hizo Bw.Jensen Kirknaes amewataka
watanzania waje kwa wingi katika onesho hilo kwani kila picha moja
inamaana chanya zaidi ya elfu moja hivyo anaamini watanzania
watajifunza Vingi kupitia onesho hilo.
No comments:
Post a Comment