• Breaking News

    ..

    ..

    Tuesday, 20 September 2016

    MBUNGE PETTER MSIGWA AMEKABIDHI MADAWATI 537


    MBUNGE wa Jimbo la Iringa mjini mchungaji
    Petter Msigwa akikabidhi madawati  537 ambayo ameyatoa kwa ajili ya jimbo la iringa mjini
    .

     MBUNGE wa Jimbo la Iringa mjini mchungaji
    Petter Msigwa akikabidhi madawati  537 akiwa na meya wa manispaa ya iringa Alex Kimbe
     MBUNGE wa Jimbo la Iringa mjini mchungaji
    Petter Msigwa akikabidhi madawati  537 akiwa na meya wa manispaa ya iringa Alex Kimbe
    haya ni baadhi ya madawati 537aliyokabidhi MBUNGE wa Jimbo la Iringa mjini mchungaji
    Petter Msingwa.
    NA FREDY MGUNDA,IRINGA
    MBUNGE wa Jimbo la Iringa mjini mchungaji
    Petter Msigwa amekabidhi madawati hayo 537 ambayo ameyatoa katika jimbo lake
    yataweza kuwa mkombozi mkubwa kutokana na kuweza kuwasaidia wanafunzi waliokuwa
    wanakabiliwa na chanagamoto ya kusoma katika mlundikano mkubwa na baadhi yao
    walikuwa  wanakaa chini ya sakafu.
    Aidha Msigwa katika hotuba
    yake ya kukabidhi madawati hayo amewataka viongozi wa manispaa ya iringa na
    tabia ya kuhujumu na kuiharibu
    miundombinu ya shule na badala yake wahakikishe wanatunza mali zote za
    serikali kwa lengo la kuweza  kuwasaidia
    watoto wengine wa vizazi vijavyo waweze kusoma katika mazingira mazuri.
    “Sipendi kuona wanafunzi
    wanaosoma katika shule za jimbo langu wanakaa chini,kitendo hicho huwa
    kinaniumiza sana ndio maana nimeamua kupambana kutafuta madawati ili
    kufanikisha adhima yangu ya kukuza elimu kwa wanafunzi wa jimbo la iringa mjini”alisema
    Msigwa
    Naye meya wa halmashauri ya
    manispaa ya iringa Alex Kimbe amesema kwamba kwa sasa hawana mapungufu yoyote
    ya madawati hivyo  hakutakuwa na
    changamoto ya mwanafunzi wake kujisomea wakiwa wamekaa chini ya sakafu.
    MADAWATI hayo 537 ambayo
    yametolewa na ofisi ya Mbunge wa Iringa Mjini yamegharimu kiasi cha zaidi ya
    shilingi milioni 60 yatasambazwa katika kata zote ambapo pia yataweza  kusaidia kwa kiasi kikubwa kuwaondolea adha
    wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ambao walikuwa wanakabiliwa na
    changamoto hiyo kwa kipindi cha muda mrefu na hatimaye  kuongeza kiwango cha ufaulu.
    Lakini tatizo la kupanda na
    kushuka kwa kiwango cha ufaulu katika baadhi ya shule za msingi na sekondari
    katika halmashauri ya manispaa ya iringa lilikuwa linasababishwa na wanafunzi
    wengine  kujisomea wakiwa wamekaa chini ya
    sakafu sambamba  na kuwepo katika
    mazingira ya  miundombinu ambayo sio
    rafiki kwao hivyo kujikuta wanashindwa kutimiza malengo yao.
    Hayo yamebainishwa na baadhi
    ya wanafunzi wa shule ya sekondari na shule za msingi katika manispaa ya
    iringa.
     Wanafunzi hao akiwemo Ayoub Joseph,Paul Kisige
    pamoja na Riziki Ismail walisema kwamba kitendo cha baadhi yao kujisomea wakiwa
    sakafuni kimepelekea kupunguza uwezo wa kifikiri na kujikuta wanafanya vibaya
    katika masamo yao na kushindwa kufaulu, hivyo wamempongeza mbunge wa jimbo la
    iringa mjini mchungaji Petter Msingwa kwa juhudi wanazozifanya za kupambana na
    adha ya  madawati.
    “Hapo mwanzoni kwa kweli
    hali ilikuwa ni ngumu sana kwa sababu wanafunzi wengine walikuwa wanasoma
    wakiwa wanakaa chini ya sakafu na hii kiukweli unamwondolea kabisa uwezo wa
    kufanya vizuri mwanafunzi, lakini kutokana na agizo hili la Rais tumepata nafuu
    kubwa na wanafunzi tuna imani tutaweza kufanya vizuri katika masomo yetu, na
    pia tunampongeza mbunge wetu kwa juhudi zake za kutuletea madawati,”walisema
    wanafunzi hao.
    Pia walisema kwamba pamoja
    na changamoto ya kuwepo kwa upungufu wa madawati lakini serikali inatakiwa
    kuhakikisha inatilia mkazo suala linguine la nyumba za walimu pamoja na
    kuimarisha mambo mengine ya msingi, kama kuongeza madarasa mwengine ili kuweza
    kuepukana na mlundikano kwa wanafunzi.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI