• Breaking News

    ..

    ..

    Monday, 24 October 2016

    MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AMEKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA ITALIA NCHINI


    Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza
    na Balozi wa Italia nchini Mhe. Roberto Mengoni (kushoto) ,Ikulu jijini Dar es Salaam
    Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi wa Italia nchini Mhe. Roberto Mengoni
    (kushoto) mara baada ya kumaliza mazungumzo ,Ikulu jijini Dar es Salaam .

    Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiagana na
    Balozi wa Italia nchini Mhe. Roberto Mengoni (kushoto) aliyemtembelea na kufanya
    naye mazungumzo  ,Ikulu jijini Dar es Salaam 

                          
    Balozi wa Italia hapa nchini Tanzania Roberto Mengoni amemhakikishia Makamu wa Rais wa
    Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuwa nchi yake itaendelea
    kudumisha na kuendeleza mahusiano mazuri na ya kihistoria kati ya nchi hizi
    mbili katika sekta mbalimbali kama hatua ya kuongeza chachu ya maendeleo kwa
    wananchi wa mataifa hayo mawili.
     
    Balozi
    huyo wa Italia hapa nchini ametoa kauli hiyo leo 24-Okt-2016 alipokutana
    na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ikulu jijini Dar es
    Salaam.
    Balozi
    huyo Roberto Mengoni ameeleza kuwa nchi yake itaendelea kushirikiana ipasavyo
    na Tanzania katika sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya afya,utamaduni na elimu.
    Kwa
    upande wake, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu
    Hassan ameishukuru Serikali ya Italia kwa kuendelea kusaidia miradi ya
    maendeleo ikiwemo ya afya hapa nchini.
    Makamu wa
    Rais amesema Serikali itaendelea kushirikiana na Italia katika sekta mbalimbali
    ikiwemo uimarishaji wa biashara na shughuli za utalii kati ya Italia na
    Tanzania.

    Amesisitiza
    kuwa Serikali ipo tayari wakati wowote kupokea mawazo mazuri ya kimaendeleo
    kutoka kwa Serikali ya Italia yatakayosaidia kujenga na kuimarisha ustawi mzuri
    katika jamii hapa nchini.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI