• Breaking News

    ..

    ..

    Thursday, 10 November 2016

    Hali Bado tete Maelfu waandamana Marekani kupinga ushindi wa Trump

    Kufuatia kutangazwa kwa Donald Trump kuwa Rais mteule wa Marekani, wananchi wa Marekani wameandamana katika miji saba kupinga ushindi huo wa Trump.

    Waandamanaji hao wamekusanyika nje ya mnara maarufu wa Trump ‘ Trump Tower’  mjini New York wakipaza sauti za kumpinga Trump. Wengine walionekana nje ya Ikulu ya Marekani wakipaza sauti kuwa “Not my president” (Si Rais wangu), pamoja na mabango mengine.

    Wengi wa waandamanaji walioongea na CNN wameelezea kuwa wana wasiwasi sana kuhusu Trump kwavile kuongoza Marekani sio kama kuiongoza nchi yoyote duniani.

    “Kwa matokeo haya tumeiangusha Dunia. Trump hakustahili kuwa Rais. Nahisi watu walipiga kura kwa hasira lakini Trump ni hatari kwa dunia,” alisema mmoja wa waandamanaji aliyejitambulisha kwa jina la James Betwell kutoka Califonia.


    Advertisement

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI