• Breaking News

    ..

    ..

    Tuesday, 15 November 2016

    Kituo cha msaada wa kisheria kwa wanawake chaitaka serikali kubadili sheria ya mirathi

    Kituo cha msaada wa sheria kwa wanawake WLAC kimeitaka serikali kurekebisha sheria ya mirathi ya kimila kwa kuwa sheria  iliyopo ni ya kibaguzi na kandamizi kwa wanawake na wototo wa kike hali inayochangia kurudisha nyuma jitihada na maendeleo yao katika kujikwamua kiuchumi.


    Hayo yamebainishwa leo jijini dar-es-salaam na mkurugenzi wa kituo cha msaada wa sheria kwa wanawake bi,Theodosia Nshala  na kueleza kuwa sheria  ya mirathi na kimila ni ya kuwakandamiza wanawake na watoto na inakinzana na katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kuwa zinashikilia mila na desturi ambazo zinamnyima mjane na mtoto wa kike fursa ya kurithi na kuongeza mashauri ya mirathi.


    ‘’tatizo la mirathi bado ni kubwa na Linahitaji jitihada madhubuti ilikuweka mazingira rafiki kwa upatikanaji wa haki kwa wajane na watoto ikiwemo kuwepo kwa sheria ya mirathi inayosimamia haki za wanawake na watoto hivyo tunaiomba serikali kubadilisha sheria hii kandamizi kwa wajane. alisema Theodosia.


    Mkurugenzi huyo alifafanua kuwa   idadi ya mashauri 811 ya mirathi yamefikishwa kwa wasaidizi wa kisheria katika mikoa ya iringa, kigoma,rukwa katika kipindi cha mwezi januari hadi oktoba 2016 huku mkoa wa mbeya ukiongoza kwa kupokea mashauri  153 ya mirathi.


    Hata hivyo aliongeza kwa kusema kuwa maamuzi ya Mahakama yameendelea kugharimu maisha ya wajane na watoto wa kike kwakuwa bado  upatikanaji wa haki za mirathi umekuwa mgumu japo mahakama inatumia busarana nguvu nyingi katika kuhakikisha haki inapatikana

    .

    ‘’serikali ijitahidi kutoa elimu kwa jamii ili kuondokana na mila potofu dhidi ya wanawake na watoto kwa kuwatendea haki badala ya kuwanyanya kwa namna mbalimbali.aliongeza mkurugenzi huyo.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI