• Breaking News

    ..

    ..

    Thursday, 3 November 2016

    Mke wa Trump amnadi mumewe hadharani



    Amesema kuwa mume wake anaipenda Marekani na ameahidi kuifanya kuwa nchi yenye nguvu kwa mara nyingine
    Image captionAmesema kuwa mume wake anaipenda Marekani na ameahidi kuifanya kuwa nchi yenye nguvu kwa mara nyingine
    Mke wa mgombea urais Marekani kupitia chama cha Republican Melania Trump, ametoa hotuba ya kampeni isiyo ya kawaida kuhusu uchaguzi utakaofanyika Jumanne ijayo novemba 8.
    Akizungumza katika jimbo la Pennsylvania, mke wa Trump alielezea majukumu yake kama mama na historia yake ya uhamiaji.
    Amesema kuwa mume wake anaipenda Marekani na ameahidi kuifanya kuwa nchi yenye nguvu kwa mara nyingine.
    Melania amesema tuhuma anazopewa mumewe juu ya unyanyasaji kwa wanawake ni uongo
    Image captionMelania amesema tuhuma anazopewa mumewe juu ya unyanyasaji kwa wanawake ni uongo
    Kwa upande mwengine Rais Obama amekuwa akiwashawishi wapigakura vijana katika jimbo la Florida kukiunga mkono chama cha Democtaic na Hillary Clinton.
    Donald Trump aliwahi kuhutubia jimboni hapo, kabla ya kwenda North Carolina.
    Bi Clinton pia ataenda kufanya kampeni jimboni hapo.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI