• Breaking News

    ..

    ..

    Monday, 14 November 2016

    MKUU WA WILAYA YA KINONDONI HAPI AMEWATAKA VIJANA WAJIAJIRI

    Watanzania wamehimizwa kuondoa fikra kutegemea kuajiriwa baada ya kumaliza masomo ya elimu juu bali wametakiwa kufikiria mbinu  za kujiajiri  kuondokana na tatizo la ukosefu wa ajira.dc-hapi-vijana-4

      Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Salum Hapi ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa  mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana wasiopungua elfu 1000 waliohitimu vyuo mbali mbali na kanda nyinginezo za  elimu ndani ya wilaya hiyo, kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kubuni biashara na miradi mbalimbali.

    Hapi amesema serikali haina uwezo wa kuajiri wanafunzi wote kutokana na ufinyu wa ajira hivyo anawataka kubuni mipango ya kujiajiri.dc-hapi-vijana-leo

    Ameongeza kuwa jukumu la serikali ni kuwawekea mazingira mazuri  wahitimu hao ili waweze kujiajiri, katika hatua nyingine DC Hapi ameanzisha mafunzo hayo kwa nia ya kuwaondoa uwoga vijana katika kujiajiri kwani amebaini vijana wengi ni waoga katika kuthubutu kujiajiri.

    Kwa upande wake vijana waliopewa mafunzo wamemshukuru mkuu huyo wa wilaya huku wakihaidi kutekeleza elimu waliyopewa kwa vitendo

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI