• Breaking News

    ..

    ..

    Tuesday, 22 November 2016

    MWENYE KITI WA SOKO LA MBANDE AOMBA KUPIGWA RISASI MBELE YA WANANCHI

     RC MAKONDA ametembelea  kata ya mbandejiji dar es salaam   kwa ajili ya kusikiliza kero za wananchi  hata hivyo mkuu wa mkoa alimpatia nafasi mwenyekiti wa soko la mbande kwa ajili ya kutoa kero alio nayomokio-hassan

     Mwenyekiti soko la Mbande Mbagala katika Halmashauri ya Manispaa ya Temeke, Mokiwa Hassani ameomba kupigwa risasi mbele ya Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam, Paul Makonda baada ya kutuhumiwa kutoza kiwango kikubwa cha fedha katika upangishaji wa vizimba
    Mwenyekiti akijitetea mbele ya Wananchi

    Mwenyekiti huyo ametoa kauli hiyo baada ya mkuuwa mkoa kufika sokoni hapo kwaajili ya kusikiliza kero zinazowakabili wananchi ikiwa ni siku ya chache za ziara yake katika jiji la dar es salaam

    Kufuatia kesi hizo ikamlazimu mkuu wa mkoa kumsimamisha mwenyekiti wa soko hilo Hassani ili kujibu tuhuma hizo ndipo alipotoa kauli hiyo na kufafanua kuwa bei hiyo ya shilingi laki nne kwa kizimba ni makubaliano kati yao na wananchi hao, pia fedha hizo zimetumika kwa ajili ya kuendesha soko hilo, ambalo bado halijakabidhiwa kwa Halmashauri.

    Kufuatia utetezi huo ikamlazimu Mkuu wa Mkoa kutumia busara ambapo ameuagiza mkuu wa wilaya ya Temeke Felix Lyaniva kusimamia uundwaji wa uongozi wa soko hilo haraka mpaka kufikia mwezi Desemba kero zinazolikabili soko hilo ziwe zimetatuliwa

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI