• Breaking News

    ..

    ..

    Sunday, 27 November 2016

    WAKAZI WA KIBAMBA WAZUIA MSAFARA WA MKUU WA MKOA PAUL MAKONDA

    Wakazi wa Kibamba Wilayani Ubungo wamezuia msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Paul Makonda huku wakiwa wamebeba mabango yanayoonesha kuwa wamedhulumiwa ardhi yao.rc-makonda-msafara-1

    Akizungumza na wakazi hao waliokuwa wamesimamisha msafara huo Mkuu wa Wilaya hiyo Humphrey Polepole amewataka wakazi hao kufuata utaratibu Kwani madai yao yamefika mezani kwake na baadhi yamenza kushughulikiwa kwa watu kulipwa fidia zao kutokana na kupisha eneo la chuo na hospitali ya MUHAS .rc-makonda-msafara-10

    DC Polepole amesisitiza kuwa serikali ipo pamoja na wAjax hao ambao wengine wanadai fidia ya eneo la kwembe na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete alihaidi kuwa watalipwa, vilevile Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alihaidi kuwa serikali itazifanyia kazi ahadi zote zilizoachwa na serikali iliyopita.rc-makonda-msafara-9

    DC Polepole ameongeza kuwa kwa wale wakazi waliopo maeneo ya hifadhi ya barabara serikali itaendelea na msimamo wake wa upanuzi wa barabara kama alivyohaidi Rais Magufuli jana kwenye Mkutano wa hadhara wa RC Makonda uliofanyika Maramba Mawili.rc-makonda-msafara-5

    Kwa upande wake RC Makonda ambaye alishuka baada ya wakazi hao kuonekana kugoma kupisha msafara hu nakuwaambia kufuata utaratibu kutokana na majibu ya awali ya DC Polepole.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI