• Breaking News

    ..

    ..

    Thursday, 1 December 2016

    MAKAMBA ;ALALAMIKIA HALI YA MAZINGIRA TANZANIA





    Waziri wa nchi ofisi ya Makamu  wa Rais Muungano na mazingira  mh January Makamba, Leo amefanya  semimina fupi na wahariri pamoja  na waandishi wa habari kuhusu hali ya mazingira nchini na kueleza kuwa tatizo la uchafuzi wa mazingira nikubwa  najuhudi za makusudi zinatakiwa  kuchukuliwa ili kuinusuru nchi  kugeuka kuwa jangwa .

    Aidha Mh Makamba amesema kutokana na ziara yake ya aliyotembelea Mkoa 10 nchini ili kujionea hali ya mazingira nchini amejionea uharibifu Mkubwa wa vyanzo vya maji ambapo katika ziwa Rukwa limeathiwa na wakulia  kina chake kinapungua kutoka mita 9 hadi 6. na safu za milima mbeya amekusudia kulitangaza kuwa eneo nyeti la uhifadhi mazingira na maeneo mengine nchini  yanayofanana na hayo  halmashauri zimeagizwa kuyawekea alama.


    Katika mkutano huo limeibuka suala la uuzaji mkaa nje ya nchi ambapo waandishi wa habari wamemuomba Waziri  kulitazama upya jambo hilo kwa kuwa  linachangia kwa kiasi kikubwa  ukataji wa miti.

    Hata hivyo Mh Makamba amewataka wahalili na waandishi kuendelea kutoa Elimu kwa jamii juu ya kuhifadhi mazingira ikiwemo kupanda miti.

    " Nimewaita Leo kuwaomba kuwaomba tusaidiane na kushirikiana kuifanaya nchi yetu na jamii yetu na watu wetu wayape kipaumbele masuala ya hifadhi ya mazingiza"  amesema Makamba.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI