Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Dkt. Adelhelm Meru akizungumza wakati wa hafla ya kufunga maonesho ya Kwazna ya Viwanda vya Tanzania yaliyomalizika jana jijini Dar es Salaam. Takribani Viwanda vidogovidogo 362 vilishiriki katika maonesho hayo ya yaliyoanza kuanzai tarehe 07 hadi 11 Desemba 2016.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji (Viwanda) Dkt. Adelhelm Meru akipokea zawadi kutoka kwa Kikundi cha Sanaa cha Albino Revolution Cultural Troupe kwa kuthamini mchango wake katika kukuza uwekezaji kwa watuwenye ulemavu wakati wa hafla ya kufunga maonesho ya Kwanza ya Viwanda vya Tanzania jana jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji (Viwanda) Dkt. Adelhelm Meru akimkabidhi Cheti cha Ushiriki wa maonesho ya Viwanda vya Tanzania mwakilishi wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Bw. James Ndege wakati wa hafla ya kufunga maonesho hayo jana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendeji wa TANTRADE Bw. Edwin Rutageruka.
: Baadhi ya washiriki wa maonesho ya kwanza ya viwanda vya Tanzania wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji (Viwanda) Dkt. Adelhelm Meru alipokuwa akifunga maonesho hayo jana jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji (Viwanda) Dkt. Adelhelm Meru akipokea zawadi kutoka Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya maonesho ya viwanda vya Tanzania Bibi. Neema Mhondo (kushoto) kwa kuthamini mchango wake katika kukuza viwanda nchini wakati wa hafla ya kufunga maonesho hayo jana jijini Dar es Salaam.
Picha zote na: Frank Shija – MAELEZO.
No comments:
Post a Comment