• Breaking News

    ..

    ..

    Sunday, 1 January 2017

    WALEMAVU WA KIJIJI CHA LULANZI WAMLILIA MBUNGE RITTA KABATI

    Mbunge wa viti maalum mkoa waIringa(CCM) Rita Kabati akiongea na familia ya watu watano wenye ulemavu wa viungo alipowatembea katika kijiji cha Lulanzi kata ya Mtitu wilayani Kilolo mkoa wa Iringa wakati wa kuwasaidia msaada kukarabati nyumba yao pamoja na kuwapa vitu vingine vya kimsaada
    Leah mwamoto mtoto wa mbunge wa jimbo la kilolo Vennance Mwamoto naye alishuhudia maisha magumu wanaoishi familia ya watu watano wenye
    ulemavu wa viungo alipowatembea katika kijiji cha Lulanzi 
    kata ya Mtitu wilayani Kilolo mkoa wa Iringa na hapo aliposimama ndio choo kinachotumiwa na familia hiyo kwa sasa huku wakisubili ujenzi wa choo kipya kinachoendelea kujengwa kwa hisani ya mbunge Ritta kabati
     Hivi ni baadhi ya vifaa vilivyoletwa na mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama
    cha mapinduzi (CCM) Rita Kabati kwa ajili ya kuwasidia 
    familia ya watu watano wenye
    ulemavu wa viungo alipowatembea katika kijiji cha Lulanzi 
    kata ya Mtitu wilayani Kilolo mkoa wa Iringa
     
    Na fredy mgunda,Iringa
     
    FAMILIA ya watu watano wenye
    ulemavu wa viungo wamemuomba mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama
    cha mapinduzi (CCM) Rita Kabati kuendelea kuilea familia hiyo kama familia
    yake.
     
    Akizungumza na blog hii
    mmoja wa wanafamilia
     hiyo,Elias Mpogole ambaye ni mlemavu alisema kuwa
    mbunge huyo amekuwa akiwasaidia toka siku ya kwanza walipokutana naye katika
    kijiji hicho cha Lulanzi.
     
    “Zamani tulikuwa tunaishi
    kwenye nyumba ambayo inavuja haina dilisha wala mlango pia tulikuwa tunalala
    chini lakini mbunge Kabati katusaidia nyumba nzuri kama mnavyoiona waandishi,katuletea
    magodoro,mashuka,blanket na sasa ameanza kutujenga choo cha kisasa na
    ameshawalipa mafundi pesa zote ndio maana tunaomba anendelee kuwa na sisi.”Alisema
    Mpogole
     
    Mpogole alishukuru msaada
    waliopatiwa na kuwataka wadau wengine waweze kujitokeza zaidi kuwasaidia
    kuwapatia vyakula na radio za kuwezakusikiliza nyimbo za dini.
     
    Kwa upenda wake mbunge wa
    viti maalum mkoa waIringa(CCM) Rita Kabati ametoa msaada wa vitu mbalimbali
    ikiwemo ukarabati wanyumba kwa familia yenye watoto walemavu wanne wa kijiji
    cha Lulanzi kilichoko kata ya Mtitu wilayani Kilolo mkoa wa Iringa. 
     
    Msaada huo wa ukarabati wa
    nyumba,umeambatana na magodoro, vyakula na ujenzi wa choo cha kisasa ameutoa
    baada yakuwahidi kufanyia matengenezo ya nyumba ambayo walikuwa wakipata shida
    kipindicha masika mara baada ya kufanya ziara mapema mwaka huu katika kijiji
    hicho nakugundua mateso wanayokumbana nayo familia hiyo. 
     
     “Nimeitembelea familia hiinimeumia sana
    kwani maisha wanayoishi ni ya shida sana hawana msaada wowotenyumba yao inavuja
    hawana chakula maishayao ni ya kuunganga unga mpaka watu  wajekama sisi kuwaletea vitu  vidogo vidogokama mchele na mafuta na mbaya Zaidi
    hata watoto hao wote watatu hakuna hatammoja aliyewahi kukanyaga shule ingawa
    wanaonekana ni wakubwa hivyo jamii tunapaswa kuwasaidia watoto hawa” alisema Kabati  
     
    Familia hiyo ambayo baba
    mzazi Mzee LucasMpogole mbaye kwa sasa amelazwa hospitali ya mkoa wa Iringa kwa
    ugonjwa wakupooza ina watoto wanne wote wakiwa walemavu wa viungo hivyo kukosa
    msaadakabisa pindi mvua zikianza kijiji hapo. 
     
    Akizungumza wakati wa
    kukabidhimsaada huo , Kabati alisema kuwa jamii ya walemavu wanahitaji msaada
    wa hali namali kutoka kwa wadau wenye uwezo na kuacha tabia ya kuiacha serikali
    peke yakekatika kutatua kero zao na kuwahudumia.
     
    Alisema kuwa msaada huo
    utawafarijiwalemavu hao waone kuwa pamoja na upungufu walionao bado jamii ya watanzaniainawathamini
    na kuwajali katika maisha yao ya kila siku.
     
     Aliongeza kuwa walemavu wanayo hakiya kuishi
    na kujitegemea iwapo jamii itawajengea uwezo badala ya kuwafungiandani na
    kuwaona kama ni mkosi katika familia ila kugundua vipajiwalivyonavyo na
    kuiwezesha serikali kuwaingiza katika mipango mbalimbali yakuwapatia huduma. 
     
    Kabati alitoa wito kwa
    serikalikuona umuhimu wa kutumia vituo mbalimbali vinavyolea watoto wenye ulemavukuhakikisha
    vinawejengea miundo mbinu rafiki na uboreshaji mipango na mfumo wautoaji elimu,
    afya na usafiri kulingana na tofauti za umri wa watoto nchini. Aidha Kabati alitoa
    wito kwa Mfukowa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kuangalia kwa jicho la tatu familia
    ya Mpogolekwa kuwaongezea kipato zaidi cha kila mwezi kwani kwa hali waliyonayo
    nakiwango wanachopata kila baada ya miezi miwili hakiendani na uwingi wa
    walemavuwa familia hiyo maskini. 
     
    Naye baba mdogo wa watoto hao
    akiongea kwa niaba ya baba mzazi wa walemavu hao, Juma Mpogole alimshukurumbunge
    huyo kwa msaada aliotoa na kumtaka awasomeshe watoto wake ambao tangu wazaliwe
    hawajawahi pata elimu yoyote licha ya kufikisha umri wa miaka zaidi 20.
     
    Lakini naomba nitoe rai kwa
    wale wanasiasa na wananchi wengine wanaokuja kupiga picha nah ii familia ya
    watu wenye ulemavu wa viungo kwa ajili ya kujitafutia umaarufu waache tabia
    hiyo.
     
    “Kila mara tunaona waandishi
    na wapiga picha wanafika hapa na viongozi mbalimbali lakini kila siku wanatoa
    ahadi tu sioni msaada wowote ule unaotolewa zaidi ya kuona wanajitafutia
    umaarufu huko mitaani naomba waacha tabia hiyo sisi tunamuona mbunge Ritta
    Kabati na kaka yake mbunge wa jimbo hili la kilolo Vennence mwamoto ndio
    wanaosaidia familia hii,kweli familia hii inaitaji msaada hivyo njooni kutoa
    msaada sio kupiga picha pekee yake”.alisema Mpogole

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI