• Breaking News

    ..

    ..

    Wednesday, 1 February 2017

    JARIDA ...............JIPYA


     
    i
    BODI YA UHARIRI
    Mwenyekiti
    Dkt.Hassan Abbasi Mkurugenzi-Idara ya Habari-MAELEZO
    Wajumbe
    Zamaradi KawawaVicent Tiganya John Lukuwi Patrick KipangulaElias Malima
    Wasanifu Jarida
    Benedict LiwengaHassan Silayo
    Huduma zitolewazo MAELEZO
    1. Kuuza picha za Viongozi wa Taifa na matukio muhimu ya Serikali,2. Kusajili magazeti pamoja na majarida,3. Kukodisha ukumbi kwa ajili ya mikutano na Waandishi waHabari,4. Rejea ya magazeti na picha za zamani,5. Kupokea kero mbalimbali za Wananchi 
    Jarida hili hutolewa na
    Idara ya Habari-MAELEZO S.L.P 8031Dar es Salaam, Simu: 022-2122771Baruapepe: maelezo@habari.go.tz Tovuti: tanzania.go.tz 
    Limeandaliwa na Idara ya Habari-MAELEZO
     
    TAHARIRI
    Tanzania ni NCHI YETU na kwa faida yetu
    Wapendwa wasomaji wa jarida hili la NCHI YETU lenye historia ndefu naTanzania yetu, ninayo furaha leo, mimi binafsi na timu nzima ya Idara yaHabari-MAELEZO, kushuhudia historia nyingine ya jarida hili kuanza kutokamtandaoni.Kama inavyofahamika, kwa miaka mingi sasa jarida la NCHI YETU limekuwalikichapishwa na nakala zake kusambazwa wakati wa maadhimisho makubwaya kitaifa tu kama vile sherehe za Muungano na Uhuru.Wakati tukiahidi kuwa machapisho hayo maalum ya siku hizo yataendelea, nifaraja kwetu leo kuona jinsi maendeleo ya teknolojia na mageuzi katika sektaya upashanaji habari, yanavyotuwezesha kulichapisha jarida hili kwa njia ya
    mitandao ili kuwakia wasomaji wengi zaidi.
    Hivyo basi, kuanzia Januari, 2017, ukiacha matoleo maalum, jarida lako hililitakuwa likitoka kila mwezi kwa njia hii na tutajitahidi kulisambaza kwa njia
    mbalimbali mitandaoni ili kuwakia wasomaji wengi.
    Tunawaahidi kuwa NCHI YETU litabaki kuwa jarida lile lile lililosheheni habarina uchambuzi muhimu kuhusu maendeleo na jitihada za nchi yetu Tanzaniapamoja na watu wake katika kujiletea maendeleo. Jarida litasheheni piamatukio muhimu yaliyotokea katika mwezi husika na litakumbushia pia historiaya nyuma.NCHI YETU pia litakuwa johari muhimu ya kuhamasisha utii kwa tunu muhimuza Taifa letu kama vile amani, utulivu, uzalendo, lugha na utamaduni. Ni jarida litakalosimama na kusimamia Tanzania tunayoitaka, na itakapobidi,tutakemea na kuonya juhudi zozote za kuzifuta tunu hizi.Ndio maana tahariri hii ya kwanza imeanza kwa kutukumbusha jambomuhimu-kwamba Tanzania ni nchi yetu na sote tuna budi na dhima yakuchangia katika maendeleo yake kwa faida yetu ya sasa lakini na vizazivijavyo.Nawatakia usomaji mwema wa jarida hili. Asanteni sana.
    Dkt. Hassan Abbasi,Mwenyekiti, Bodi ya Uhariri,Mkurugenzi-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali
    ii
    Limeandaliwa na Idara ya Habari-MAELEZO

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI