• Breaking News

    ..

    ..

    Thursday, 30 March 2017

    Mahakama kuu Dar yamuachia huru Mbunge Lijuakali

    Mahakama Kuu kanda ya Dar es Salaam imetengua hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Wilaya Kilombero dhidi ya Mbunge Peter Lijualikali(Chadema) baada ya kukubaliana na warufani kwamba hati ya mashtaka iliyomtia hatiani  ilikuwa na upungufu.

    Uamuzi huo umetolewa Alhamisi hii mbele ya Jaji Ama- Isaria Munisi baada ya kupitia sababu za kupinga mbunge huyo kutiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo cha miezi sita jela. Peter aliwakilishwa mahakamani na Wakili Tundu Lissu na Fred Kiwelo wakati Jamhuri ilikuwa ikiwakikishwa na Wakili wa Serikali, Faraja Nchimbi.
    Mbunge Lijualikali na Dereva wake, John Kibasa walihukumiwa kwenda jela miezi sita bila faini kwa kosa la kufanya vurugu na kusababisha taharuki katika maeneo ya ukumbi Wa halmashauri ya Wilaya ya Kilombero wakati wa kipindi cha uchaguzi mwaka 2015.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI