Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na
Mazingira, Luhaga Mpina amewataka viongozi wilaya ya Ilala kuwachukulia hatua
kali watu wanaokaidi kutunza mazingira yanayowazunguka.
Amesema kuwa ili kuweza kuhakikisha zoezi hilo linatimia na
kuwashirikisha wananchi wote, ni lazima viongozi wawachukulie hatua kali wananchi ambao wanakaidi
kushiriki katika zoezi hilo kwa lipo kwaajili ya kuiokoa jamii na magonjwa mbalimbali ya
mlipuko.
"Ninyi viongozi mnatakiwa kuwachukulia hatua kali wale
wananchi wachache wanaokaidi kushiriki katika usafi, kwani haiwezekani watu
wailaumu Serikali kwa kila kitu, sisi viongozi wa juu tuleteeni wale
walioshindikana ili tuweze kuwashughulikia,”amesema Luhaga.
Aidha, katika hatua nyingine, Luhaga amewataka wananchi
kuunga mkono hatua za zinazochuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. John Magufuli kwani anania ya dhati kuleta maendeleo ya nchi.
Hata hivyo, pamoja na hayo, Mpina ameongeza kuwa katika
awamu hii ya TanoTanzania imepata Rais wa kipekee ambaye amekuwa mfano wa
kuigwa barani Afrika na duniani kote.
No comments:
Post a Comment