• Breaking News

    ..

    ..

    Monday, 7 August 2017

    Nanenane yapamba moto lindi

    Na Mathias Canal,
    Lindi

     
    Maonyesho ya Nanenane Kanda ya Kusini ambayo yalianza tokea
    tarehe 1/8/2017 katika viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi yanaendela kushika kasi
    huku kivutio kikubwa ikiwa ni baaada ya bidhaa mbalimbali zinazoonyeshwa kwenye
    mabanda na Halmashauri mbalimbali kutoka mikoa yote miwili inayounda kanda ya
    kusini ambayo ni Lindi na Mtwara.
     
    Kwa ujumla wake maonyesho ni mazuri kwani yamehusisha
    shughuli nyingi za Kilimo, Uvuvi na mifugo kama kauli mbiu inavyosema “Zalisha
    kwa Tija Mazao na Bidhaa za Kilimo Mifugo na Uvuvi ili kufikia Uchumi wa Kati” kauli mbiu hii ikiwa na
    msisitizo na hamasa zaidi kwa wananchi kutambua mbinu bora za Kilimo Mifugo na
    Uvuvi ili kuwa na kipato kikubwa kitakachopelekea wananchi kwa ujumla wao
    kufikia uchumi wa kati.
     
    Pia kumekua na wajasiriamali wengi sana ambao wamefika
    katika Maonesho hayo wakiwa na bidhaa mbalimali zikiwemo bidhaa za ngozi,
    mikoba, viungo, asali, vyakula vya asili, mashine Ndogondogo na vingine vingi
    vya kuvutia.
     
    Maonyesho ya mwaka huu yamekua chachu na kuwa na mvuto
    mkubwa kwani tangu kufunguliwa kwake kumekuwa na mgeni rasmi anayetembelea kila
    siku ambao ni mwaaziri, ama wakuu wa mikoa kutoka katika mikoa husika jambo
    ambalo limefanya maandalizi kuwa makubwa na mazuri zaidi.
     
    Kanda ya kusini ina fursa nyingi za kiuchumi
    kama vile Hali ya hewa nzuri, na Uzalishaji mazao mbalimbali hususani zao kubwa
    la Korosho, Jambo la msingi ni kujipanga vizuri
    na kuhakikisha tunatumia fursa hizi
    kikamilifu ili kupunguza umasikini na kuleta utajirisho.
     
    Katika hotuba nyingi zinazotolewa na wageni
    mbalimbali wanaozuru katika Maonesho hayo ni kuhusu Tatizo kubwa linalokabili
    sekta ya kilimo na ufugaji nchini kwa wahusika kutozingatia kanuni bora na za
    kisasa za kilimo na Ufugaji.
     
    Hivyo katika maonesho haya kuwapo kwa Taasisi
    za utafiti zinazozalisha mbegu za kisasa, Kuwapo kwa teknolojia na zana za
    kilimo za kisasa ni njia mojawapo ya kuongeza tija kwa jambo ambalo
    litawasaidia wananchi kufahamu zaidi kanuni bora za kilimo.
     
    Ufugaji nyuki ni fursa mpya ambayo endapo
    Watanzania wataichangamkia itawaletea kipato na kuwaondolea umasikini. Fursa
    haihitaji gharama kubwa kuazisha gharama kubwa ni kununua mizinga na kuweka
    maeneo rafiki ya nyuki ili waweze kuingia.
     
    Baada ya hatua hiyo hakuna gharama yeyote zaidi
    ya kuvuna na kuchakata asali ili iwe na ubora wa kimataifa.
     
    Nyuki wanatoa mazao mengi ikiwa ni pamoja na
    nta ambayo inatumika kutengeneza mishumaa na bidhaa nyingine.
     

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI