• Breaking News

    ..

    ..

    Friday 11 August 2017

    SHULE YA ALMUNTAZIR YAWAONGOZA WANAFUNZI WA SHULE BINAFSI BARANI AFRIKA KATIKA KUSHIRIKI MDAHALO WA ELIMU

     Mkurugenzi wa shule za almuntazir islamic school,akizungumza na waandishi wa habari leo jijini dar es salaam.


     huyu ni katibu wa mshindano hayo yajulikanayo kama Mwalimu Nyerere school invetation debate championship Bwn. Dominic Mwakifulefule.




    ,

     hawa ni wanafunzi waliopata nafasi kushiriki katika mdahalo huo,wakati wakijadiliana ukumbini hapo.

     
    hawa ni baadhi ya wanafunzi walioshiriki mashindano hayo Mduduzi Mhlanga kutoka Zimbabwe(kulia) pamoja na mwanafunzi kutoka alimuntazir( kushoto).




    Wanafunzi 250 kutoka katika shule mbalimbali za afrika kushiriki katika Mashindano ya mdahalo yaliyoanza leo katika shule ya Almuntazur seminary school, iliyopo jijini dar es salaam kwa  lengo La kuwajengea wanafunzi hao uzoefu wa kijieleza kwa kumjenga mwanafunzi katika kujiamini na kuweza kufanya vizuri katika soko LA ajira.

    Akizungumza na waandishi wa habari mkurungenzi wa shule zote za Almuntazir Islamic school bwn. Mahmood Ladak, amesema , mashindano hayo ambayo yameshirikisha shule 15 kutoka Tanzania na nyingine kutoka katika nchi nyingine kama Zimbambwe,South Afrika pamoja  na Uganda.

    Amesema kuwa  kwa lengo LA mashindano hayo ni kuwakutanisha wanafunzi hao na kutoka shule nyingine ili kunadilishana mawazo mbalimbali ya kielimu waliojifunza darasani.

    Mashindano hayo yajulikanayo kama Mwl Nyerere school inventation debate championship,  yanayotarajiwa kumalizika August 13 mwaka huu.

     katika mjadala huo kuna mada mbalimbali ambazo wanajadili ikiwemo National system na mada mbalimbali zinazohusu masomo na kuwapa  fursa wanafunzi hao kubadilishana mambo mbalimbali waliyojifua katika masomo yao.

     Kwa upande wake Mratibu wa Mdahalo Dominic Mwakifulefule amesema katika kuandaa mdahalo huu walitumia utaratibu wa kujiandikisha  (process registration) , mitando ya kijamii vyombo vya habari kwa lengo la kuhamasiaha ushiriki wa shule.

    Hata hivyo wanafunzi walipata fursa ya kuzungumza kuhusiana na mashindano hayo ambapo mwanafunzi Mduduzi Mhlanga kutoka katika shule ya st john collage Zimbabwe amesema mashindano hayo ni mazuri kwani yanawajenga katika kujieleza na kujiamini, naye mwanafunzi Hawa kutoka katika shule ya Almuntazir iliyopo Tanzania ameshukuru uongozi wa shule hiyo kuandaa mashindano kama hayo kwani yatawajenga kielimu katika masomo yao

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI