• Breaking News

    ..

    ..

    Wednesday 30 August 2017

    Ulinzi Mitanadoni unahitajika,

    >
    > Na Jonas Kamaleki – MAELEZO
    >
    > Serikali kushirikiana na sekta
    > binafsi wanaweza kujenga msingi wa kitaifa katika kuimarisha
    > Usalama katika ulimwengu mzima kwa ujumla na kudondokana na
    > uhalifu wa kimitandao.
    >
    > Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam
    > na Naibu Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mhe. Matt
    > Sutherland wakati wa ufunguzi wa Warsha ya masuala muhimu
    > katika kuweka miondombinu ya kiusalama katika mitandao.
    >
    > Sutherland amesema kuwa uhalifu wa
    > kimitandao haungalii mipaka ya nchi bali unaweza kutokea
    > mahali popote na wakati wowote. Alisisitiza hilo amesema
    > kuwa mwezi Mei mwaka huu shambulio la kimtandao lilipiga
    > mifumo karibu nchi 100 Duniani..
    >
    > “Katika shambulio hilo, Uingereza
    > tuliathirika sana hasa katika sekta ya Afya ambapo kompyuta
    > katika Hospitali nyingi zilishindwa kufanya kazi na
    > kusababisha madaktari kushindwa kupata taarifa za wagonjwa,
    > ” alisema Sutherland .
    >
    > Ameongeza kuwa Septemba mwaka jana
    > wakati lilipotokea tetemeko la ardhi Mkoani Kagera,
    > Uingereza ilikuwa mstari wa mbele katika kurejesha
    > miondombinu ya shule ya sekondari Ihungo kwani katika tukio
    > hilo waliotharika zaidi ni wanafunzi.
    >
    > Akiongelea suala la kiusalama, Naibu
    > Balozi huyo amesema kuwa katika Mkutano wa Kilele
    > utakaofanyika mwakani utangalia masuala mbalimbali ya
    > kiusalama ikiwemo kupambana na ugaidi wa kimataifa,uhalifu
    > wa makusudi, mashambulio ya kimtandao utumwa mambo leo
    > na vitisho vya demokrasia.
    >
    > Kwa upande wake, Mwezeshaji wa Warsha,
    > Dkt. Martin Koyabe kutoka Shirika la Mawasiliano la Jumuiya
    > ya Madola (CTO) amesema kuwa lento la Warsha hii ni
    > kuwawezesha watumishi wa umma na wa sekta binafsi kufahamu
    > miondombinu ya kiusalama katika sekta muhimu za kiuchumi ili
    > kuleta maendeleo nchini.
    >
    > Aidha, Dkt Koyabe amesema kuwa warsha
    > hii inakusanya watumishi pamoja ili kuwa uelewa wa kuainisha
    > maeneo muhimu ya kiuchumi yanayotakiwa mifumo yake ya
    > kimitandao kulindwa ili uchumi usiathirike endapo mifumo
    > hiyo inashambuliwa.
    >
    > “Serikali ni muhimu kutunga sera,
    > sheria na kanuni za kuweka ulinzi wa kimitandao ili
    > tusiathirike wakati shambulio linapotokea,” alisema Dkt.
    > Koyabe
    >
    > Ameongeza kuwa zipo changamoto kadhaa
    > katika kutekeleza programu za ulinzi wa kimitandao.
    > Amezitaja changamoto hizo kuwa ni ufinyu wa bajeti, uhaba wa
    > wataalaam na utaalaam katika eneo la ulinzi wa kimitandao.
    >
    > Warsha hii ni mwendelezo wa juhudi za
    > Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na CTO katika
    > kukamilisha Mkakati wa Kitaifa wa Usalama wa Kimitandao
    > (National Cyber Security Strategy)

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI