Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam Paul Makonda leo amepokea mifuko ya simenti elfu 10,000 kutoka benki CRDB kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi za Walimu .
Baada ya ziara ya kukagua ghala la kuifadhia vifaa vya ujenzi wa ofisi za walimu leo katika eneo la Jeshi Mgulani ambapo amekabidiwa mifuko ya Simenti 10,000kutoka benki ya CRDB
Paul Makonda ameendelea kuishukuru CRDB Bank kwakuendelea kuunga mkono juhudi za ujenzi wa ofisi za Waalimu na kupitia dawati ambalo wamelianzisha la uchangiaji ujenzi huo anaimani kwamba utaleta tija kwa watanzania na hususani kwa wakazi wa Mkoa wa Dsm.
"Tunatoa shukurani nyingi kwa Benki ya CRDB kwa kujitoa katika mchango wao wa milioni 100 ambapo fedha hiyo imetumika kununua mifuko ya cement" amesema.
Aidha ameyataka Makampuni kuiga mfano wa benki hiyo kwani wakifanya hivyo kwa upande wa vifaa vya ujenzi haitokuwa shida na amewapongeza kwa kuwa pamoja na Serikali na kumuunga mkono Rais John Magufuli
No comments:
Post a Comment