• Breaking News

    ..

    ..

    Friday, 15 September 2017

    MADIWANI 6 WASHIKILIWA NA POLISI

    Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Geita Mponjoli Mwabulambo akielezea juu ya hatua ambayo amechukua kwa kuwakamata madiwani sita pamoja na katibu wa UVCCM  Kutokana na kufanya maandamano ambayo yalikuwa ni kinyume na sheria za Nchi mbele ya waandishi wa habari.

    Baadhi ya askari pamoja na wafanyakazi wa mgodi huo wakiwa kwenye Bomba ambalo limepasuliwa na Madiwani wa Halmashauri kwa maelezo ya wananchi ambao waliwaona wakifanya uharibifu huo.

    Sehemu ya Bomba iliyoharibiwa ikitilili9sha maji kwa kasi kubwa zaidi kutokana na tukio ambalo limetokea siku ya jana kwa madiwani kuandamana wakishinikiza mgodi kuwalipa kiasi cha Dola Milioni 12.65 ambazo ni deni la mwaka 2004 hadi 2013. .

    Meneja Mhandamizi wa Maswala ya Jamii Mgodi wa GGM ,Manase Ndoloma akiwa sehemu ya eneo ambalo lilifanyiwa uharibifu wa kupasuliwa kwa bomba ambalo ndio linapeleka maji kwenye chanzo cha maji mgodini hapo.

    Shughuli za ukarabati wa Bomba hilo zikiendelea.

    Mafundi wakiendelea na shughuli za ukarabati wa Bomba hilo.





           
    ,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
    Madiwani 6
    wanashikiliwa na Polisi mkoani Geita baada ya kufanya maandamano kinyume cha
    sheria na kusababisha uharibifu wa Bomba la Maji la kutoka Nungwe kwenda kwenye
    Mgodi wa Dhahau wa GGM.
    Kamanda wa
    Polisi mkoani Geita Bw Mponjoli Mwabulambo amesema walichofanya madiwani hao
    jana hakikubaliki kisheria na kwamba hawakufuata utaratibu wa kufanya maandaman
    yao na kwamba wanaendelea na msako wa kuwabahini wale wote ambao wamefanya
    kitendo cha kuandamana na kusababisha baadhi ya kazi kusimama siku yjana.
    Amesema
    miongoni mwa wanaoshikiliwa  ni pamoja na
    Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM UVCCM
    wilaya ya Geita kwa tuhuma za kushiriki maandamano na kufanya uharibifu
    huo.
    “Kwa mtu wa
    kawaida sidhani kama alipendezwa na kitendo hicho tuache habari ya kuremba na
    kupepesa macho lile tukio sidhani kama ni kitendo kizuri, ni kosa ambalo
    walilitenda na kwamba tunawashikilia madiwani sita akiwemo katibu wa umoja wa
    vijana wa chama cha mapinduzi wilaya ya Geita na hicho hakikuwa kizuri lakini
    pia kukimbia kwao niseme sio suluhisho tutawakamata”Alisema Mponjoli.
    Meneja
    Mwandamizi wa Mahusiano ya Jamii kwenye mgodi wa GGM Bw Manase Ndoloma amesema
    taarifa za kupasuliwa kwa bomba hilo linalotoa maji safi  kutoka ziwa Victoria kupitia kwenye kijiji
    cha Nungwe hadi  kituo cha usambazaji
    maji kwenye Bwawa la Nyakanga walizipata kwa wananchi na ameahidi kuendelea
    kushirikiana na wananchi katika kuleta maendeleo kwenye maeneo yao na kwamba
    mgodi haujaathirika kwa kutobolewa kwa bomba hilo.
    “Tungependa
    kufanya shughuli zetu za kutekeleza miradi ya kuisaidia jamii ya Geita kwa hali
    ya usalama lakini pia kwa usalama wa wafanyakazi wetu mgodi wa dhahabu wa Geita
    utaendelea kushirikiana kwa ukaribu na serikali ya jamhuri ya muungano wa
    Tanzania pamoja na jamii inayozunguka eneo la mgodi ili kuharakisha urejeshaji
    wa maji pamoja na amani kwa ujumla ndani ya mji wa Geita”Alisema Manase.
    Mwenyekiti
    wa Kijiji cha Nungwe Bw  Revocatus Masatu
    amesema aliwaona watu kutoka halmashauri na magari ya serikali na hakuwa na
    taarifa yoyote kuhusu kupasuliwa kwa bomba hilo kwani alijua ni taratibu kwa
    halmashauri kutembelea vijiji vyake

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI