• Breaking News

    ..

    ..

    Wednesday, 13 September 2017

    Rais Magufuli afuta umiliki wa shamba hili la Manji, aivunja na mamlaka ya KDA

    RAIS  Dk. John Magufuli, ameivunja  Mamlaka ya  Uendelezaji Mji wa Kigamboni (KDA) na kutangaza  kufuta umiliki wa maeneo mawili  likiwemo lililokuwa likimilikiwa na mfanyabiashara Yusuf Manji.


    Mbali na eneo hilo la Manji lenye ukubwa wa ekari 715  eneo lingine ambalo  rais ametangaza kufuta umiliki wake ni lenye ukubwa wa ekari 5400  lililopo Pemba Mnazi wilayani Kigamboni  lililokuwa linamilikiwa na kampuni ya   Amadori .

    Rais Dk. Magufuli ameelekeza maeneo hayo sasa kuwa ni  hifadhi ya ardhi ya serikali ambapo yatapingiwa matumizi  mengine.

    Hatua hiyo ya Rais,  ilitangazwa  Dar es Salaam, leo  na  Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya  Makazi, William Lukuvi,  wakati akihutubia mkutano uliohusisha watendaji wa juu wa  Wizara, Mkoa wa Dar es Salaa na wilaya ya Kigamboni.


    Waziri Lukuvi amesema,  rais ameridhia kufutwa kwa KDA na kuelekeza  kazi zote zilizokuwa zikifanywa na  mamlaka hiyo sasa zitekelezwe na  Halmashauri  ya Manispaa ya Kigamboni.

    "Pia rais  ameagiza    wananchi wote walio katika maeneo yaliyopimwa  kukabidhiwa hati zao  na kuruhusu wananchi wilayani humo kuendeleza makazi na maeneo yao kuanzia sasa," alisema Waziri Lukuvi.

    Aidha ametoa taarifa kwa wananchi wote juu ya shamba la AMADORI  kuto fanya shughuli yeyote katika mpaka maelekezo yatakapo tolewa.

    Na shamba ambalo lilikuwa likimilikiwa mfanyabiashara Yusufu Manji limechukuliwa na serikali mara baada yakushindwa kuliendeleza kwa muda mrefu wa zaidi ya miaka 10.

    Waziri Lukuvi ameeleza kuwa mamlaka ya KDA ifanye makabidhiano ndani ya miezi sita na nyaraka zote zipelekwe ofisi ya Mkurugenzi na watoe ushirikiano kwa Halmashauri ili waweze kushirikiana vyema na Halmashauri katika kuuendeleza mji wa Kigamboni.

    Waziri Lukuvi ameeleza kuwa serikali itazidi kuchukua hatua kwa maeneo yasiyoendelezwa na kuwa mapori, huku akiwataka wenyeviti wa serikali za mitaa kuwa waangalizi na kufanikisha kuwa hakuna raia yeyote anayejenga Kigamboni bila kufuata taratibu.

    Akizungumza baada ya maamuzi hayo ya Rais Mbunge wa jimbo la Kigamboni Faustine Ndugulile ameeleza sasa umefika wakati wa wanakigamboni kufurahia kuishi kigamboni na wataweza kukopesheka na kuuza maeneo yao, huku akiisisitiza mamlaka ya halmashauri kufanikisha kuwa mji huo unapangwa vyema na kuhakikisha unapimwa na hati zinatolewa kwa wakati.

    "Tumeangaika sana tangu mwaka 2008 lakini tunatoa pongezi kwa Rais kwa kusikiliza kero yetu ya muda mrefu sasa wanakiga,boni wataweza kuuza maeneo yao na kukopesheka.


    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI