• Breaking News

    ..

    ..

    Sunday, 24 September 2017

    Serikali, tupo tayari kumsadia lisu kwa kila njia

    Msemaji wa Serikali Dkt. Hassan Abbas amefunguka na kusema kuwa hakuna masharti yoyote serikali imeweka ili Mbunge wa Singida Mashariki Mhe. Tundu Lissu apatiwe matibabu na kusema wanasubiri maombi ili waweze kugharamia matibabu ya Lissu. 
     
    Msemaji wa serikali amesema hayo jana kupitia mtandao wake wa twitter siku moja baada ya Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe kusema kuwa alipata taarifa kutoka kwa wasaidizi wa Spika wa Bunge kuwa wapo tayari kugharamia matibabu ya Tundu Lissu kwa masharti ya kuwa mgonjwa lazima apelekwe India, wapate barua ya maombi na kupata ripoti ya madaktari jambo ambalo Mbowe anasema alilikataa na kusema hawezi kufanya hivyo. 

    Kufuatia kuwepo kwa taarifa hizo ndipo Msemaji wa Serikali ameibuka na kusema kuwa hakuna masharti yoyote ambayo wameyaweka na kusema serikali ipo tayari kugharamia matibabu ya Tundu Lissu na kuwa wao wanasubiri barua kujua gharama za matibabu. 

    "Hakuna sharti lolote, tunasisitiza tena na bado tunasubiri, leteni barua rasmi tujue gharama na itifaki nyingine za tiba. Tutagharamia" alisema Dkt. Abbas 

    Aidha Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy Mwalimu aliendelea pia kufafanua jamb

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI