• Breaking News

    ..

    ..

    Saturday, 28 October 2017

    Naibu Waziri wa mifugo na uvuvi awatahadharisha wafugaji

     Naibu waziri wa Mifugo  na Uvuvi, Abdallah Ulega  amewatahadhalisha wafugaji waliopanga kuwadhuru  wananchi waliotoa taarifa  zilizosaidia Serikali kukamata mifugo iiliyoingia nchini kinyume cha Sheria hivi karibuni.

    Naibu waziri huyo ametoa tahadhari hiyo leo wakati akizungumza  na wakazi wa kata za Mgagao na  Kirya  zilizopo wilaya  Mwanga mkoani Kilimanjaro.

    Amesema Serikali haitawavumilia watu wa aina hiyo na kwamba vyombo vya ulinzi na usalama  vipo makini na kuhakikisha  usalama wananchi wa eneo.

    Amesema Serikali  ipo makini  na ina macho na masikio  ya kutosha na ipo kila mahali na kwamba kama kuna mpango mbaya dhidi ya wananchi waliotoa taarifa hizo hautafanikiwa.

    "Jambo  limeshapita acheni kutafuta mchawi. Mkae mkijua  kwamba Serikali  ina mkono mrefu atakayethubutu  kutenda mambo ataishia kwenye vyombo vya dola," amesema Ulega.

    Ulega amedai kupata taarifa  za kuwapo kwa baadhi ya wafugaji kuanza vikao  vya kumtafuta mchawi aliyetoa taarifa hizo

    Mbali na hilo, naibu waziri huyo amesisitiza kuwa Serikali  ya Rais John  Magufuli  ipo makini na imelenga kuwatetea wanyonge  na kwamba, haina nia ya kuchukua mifugo ya wafugaji  kwenye mchakato wa upigaji wa chapa.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI