DK Shika akiwa kwenye mnada uliopita
Aliongeza “Baada ya kujiandikisha, tutakujazia fomu maalumu ya kushiriki mnada, tutakuchua taarifa mbalimbali kutoka katika vitambulisho vyako vya Taifa, leseni ya udereva au pasi ya kusafiria.”
“Kama kweli wewe ni mshiriki halali tutakutaka utoe Sh2 milioni kupitia akaunti ya Yono kama dhamana ya ushiriki kuwa unataka kununua nyumba, ukishinda mnada hiyo Sh2 milioni ni sehemu ya malipo na kama ukishindwa kupata mali au bidhaa tunakurudishia mara moja,” amesema.
Amesema kwa atakayeshindwa kupata mali na Sh2 milioni ametoa na kisha akaharibu mnada, hatarudishiwa fedha na hatua za kisheria zitachukuliwa. Amesema mshindi wa mnada atatakiwa kulipa papo hapo malipo ya awali ya asilimia 25.
“Kama utasema ziko Kenya ziko wapi, tutakuchukua chini ya ulinzi kwenda benki mama, baba umeshinda nyumba lipa. Mnada tutaurudia palepale na asilimia 75 ya yule mshindi atatakiwa kulipa la sivyo fedha aliyotoa awali ya asilimia 25 haitarudishwa,” amesema Kevela.
No comments:
Post a Comment