• Breaking News

    ..

    ..

    Tuesday, 21 November 2017

    Wasifata maadili katika Teknologia ya habari na mawasiliano kuchukuliwa hatua kali

    Na Stahmil Mohamed.
    Wataalamu wa teknologia ya habari na mawasiliano(TEHAMA)wametakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na ili kutovunja amani iliyopo nchini.
    Hayo yamesemwa na Naibu waziri wa uchukuzi na mawasiliano Mhandisi Atashita Nditiye alipokuwa akizungumza na wataalamu wa sekta ya habari na mawasiliano alipotembelea katika kitengo hiko kwa Mara ya kwanza tangu alipoteuliwa kwenye nafasi hiyo ambapo ameahidi kushirikiana kikamilifu na sekta hiyo habari na mawasiliano katika mambo mbalimbali ya kukuza uchumi wa taifa pia kwa kuwadhibiti wataalamu wa kweli wa sekta ya mawasiliano kuendana na maadili ya kazi pamoja na sheria zilizopo kikamilifu ili kuepusha migogoro mbalimbali kwakuwa sekta ya mawasiliano ni kubwa na inategemewa na jamii katika kuwahabarisha na kuwapa taarifa mbalimbali zinazotokea hivyo kama maadili ya kazi pamoja sheria hazitafuatwa machafuko yanaweza kutokea.
    Aidha Mhandisi Nditiye amedhamiria kuwachukulia hatua Kali za kisheria kwa wataalamu wa mawasiliano wasiofata maadili ya kazi pamoja na kuwadhibiti wataalamu feki wa sekta ya mawasiliano kwakuwa hao ndio wanaoifanya sekta ya mawasiliano kudharauliwa kwa kutokufata maadili.
    Pia ameongeza kwa kusema kuwa watahakikisha wataalamu wa sekta ya mawasiliano wanasajiliwa haraka ili watambulike kwa urahisi kwakuwa ni taaluma tegemezi nchini.
    Naye katibu mtendaji wa kitengo cha Teknologia ya mawasiliano Mhandisi  Samson Mwella amesema sekta ya mawasiliano ni sekta ambayo imekuwa kwa 13% na ni sekta ambayo inamechangia uchumi wa nchi kwa 2%japo kuwa kunachangamoto mbali mbali zinajitokeza na anaamini changamoto hizo zikitatuliwa kikamilifu  sekta ya mawasiliano inaweza kuchangia uchumi wa nchi kwa asilimia kubwa zaidi kama ilivyo kwa nchi nyingine.
    Aidha Mhandisi Mwella ameongeza kwa kusema kuwa sekta ya mawasiliano ni sekta ambayo inatoa ajira za moja kwa moja kwa watu mbalimbali wanaojishughulisha  hivyo anaitaka serikali iwaezeshe wataalamu wa mawasiliano kwani imegundulika katika bidhaa laki moja zinazozalishwa katika viwanda  bidhaa nne zinatokana na tehama sawa na 0.004%hivyo hakuna budi kutilia mkazo katika sekta hiyo.pia amesema wataalamu wameamua kuanza kupanua wigo wa kufikisha mawasiliano kwa lugha ya kiswahili na picha ili iwafikie kwa umma wote kwa urahisi kwa wasiojua lugha pia kwa watu ambao hawasikii au kuelewa kwa lugha maandishi.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI