• Breaking News

    ..

    ..

    Monday 29 January 2018

    Ang'oa paa la nyumba kumfukuza mkewe

    Mwanaume mmoja aliyejulikana kwa jina la David Kinyua mkazi wa Gichiche nchini Kenya ameng'oa mabati ya nyumba anayoishi mke wake ambaye anadai amempangisha, akimtuhumu amekaa muda mrefu ndani ya nyumba hiyo kinyume na makubaliano.
    Kwenye tukio hilo ambalo limeleta sintofahamu kwa majirani, limeelezwa kwamba Bwana Kinyua ambaye ni mume wa Juliet Karimi alifanya tukio hilo, ili mke wake huyo aweze kuhama na kupisha mpangaji mpya.
    “Nilipanga kukarabati nyumba baada ya Julieti kutoka, ili mpangaji akija akute nyumba yenye hali ya kupendeza, lakini amekataa kutoka, na alisaini makubaliano kama mpangaji kufuata utaratibu”, amesema bwana Kinyua.
    Upande wa mke wake Bi. Juliet Karimi ambaye ndiye mke alikutwa na balaa hilo, amesema ameshangaa kuona watu wamekuja kutoa paa la nyumba kwenye nyumba anayoishi, na hata haelewi ni kwa namna gani aliishia kuwa mpangaji kwenye nyumba aliyoshiriki kujenga.
    'Nilichangia kiuchumi kwenye kujenga nyumba hii, nashangaa haya yanatokea, naomba wanaohusika na masuala ya sheria inisaidie nipate haki yangu”, amesema Julieth ambaye amepangishwa kwenye nyumba aliyoshiriki kujenga yenye vyumba vinne.
    Majirani wa wawili hao wamesema wanamfahamu Juliet kama mke wa David, na sio mpangaji kama anavyodaiwa.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI