Na Stahmili Mohammed.
Akiongea
na waandishi wa habari kuhusu hatua hiyo ya kutoa msaada kwa watoto
wanaokaa mazingira magumu, mwenyekiti kutoka kikundi cha furaha
Abdilkareem Mohammed amesema kuwa lengo lao kubwa ni kujikwamua kwenye
mazingira magumu na ikiwezekana kusiwepo kabisa na watoto tegemezi.
"Lengo
letu kuu ni kujikwamua kutoka kwenye mazingira magumu na kufuta kabisa
uwepo wa watoto tegemezi kwenye jamii yetu" amesema Abdilkareem.
Aidha
katibu kutoka kikundi cha tuamke, Nasma Shabani amesema kuwa wanafanya
hivyo kwa sababu watoto yatima wanaoishi kwenye mazingira yanayoonekana
na yanayoizunguka jamii hivyo itapelekea wao kuondokana na upweke na
kujisikia furaha kama watoto wengine wanaoishi mazingira ya kawaida.
Pia
Nasma amesema kuwa changamoto kubwa wanayokumbana nayo ni ugumu
wanaoupata pindi wanapowakusanya watoto ili kiwaweka eneo moja Na
kuongeza kuwa watoto hao hupatikana kwa njia ya kupita mtaa kwa mtaa na
nyumba hadi nyumba.
"Changamoto
tunayokumbana nayo ni kuwakusanya watoto na kuwaweka eneo moja Na
tunawapata watoto hawa kwa kutembea nyumba kwa nyumba Na kuzunguka mtaa
kwa mtaa" amesema Nasma.
Kwa
upande wake mtoto Abdalah Mussa anayesoma darasa la saba ambaye ni moja
ya watoto waliopata msaada Leo amesema kuwa amefurahi kupokea vifaa
vipya vya shule na kusema kuwa vitapelekea yeye kufanya kufanya vizuri
kwenye masomo yake.
No comments:
Post a Comment