Nyota wa klabu ya Paris Saint Germain Neymar jr ameendelea kuwa kwenye
tetesi kubwa za kurudi nchini Hispania na Rais wa La Liga Javier Tebas
amesema anatamani kumuona nyota huyo akirejea kwenye ligi hiyo.
Neymar ambaye alisajiliwa na PSG kutoka Barcelona Juni 2017 hadi sasa amefanikiwa kufunga mabao 26 kwenye mechi 24 alizoichezea timu hiyo.
Kwa upande mwingine bosi huyo wa La Liga amewahakikishia wanahabari kuwa msimu ujao wa ligi 2018/19 hakutakuwa na matatizo ya uamzi kwenye baadhi ya matukio kwasababu teknolojia ya VAR itaanza kutumika nchini humo
No comments:
Post a Comment