Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini nchini RITA, imesema, ndoa zote
zilizofungwa bila kuzingatia sheria ya ndoa ikiwemo viongozi wa dini
waliofungisha ndoa hizo kutokuwa na Leseni ya kufungisha ndoa huenda
zikabatilishwa.
Barongo ameongeza kuwa kiongozi wa dini atakayebainika kufungisha ndoa bila kuwa na Leseni ya serikali anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria kwa mujibu wa sheria ya ndoa ambayo imeipa Rita mamlaka ya kisheria, kusajili ndoa zote zilizofungwa kihalali.
Kwa upande mwingine amesema tayari serikali imewakumbusha viongozi wote wa dini kuhakikisha wanakamilisha taratibu za kukata Leseni ya kufungisha ndoa kabla ya kufungisha ndoa yoyote nchini
No comments:
Post a Comment