• Breaking News

    ..

    ..

    Wednesday 31 January 2018

    Wanamitindo wa Tanzania wameungana na kuanzisha chama chao ili kuendeleza na kukuza maslahi ya sekta ya mitindo nchini.

    Na Stahmil Mohamed
    Wanamitindo wa Tanzania wameungana na kuanzisha chama chao ili kuendeleza na kukuza maslahi ya sekta ya mitindo nchini.

    Chama hiko cha mitindo kitakachojulikana kama Fashion Association Tanzania kinalengo la kuendeleza maslahi ya sekta ya mitindo kwa kuwaunganisha ili kugawana ujuzi,uzoefu na rasilimali za sekta hiyo ya mitindo nchini.

    Hayo yamesemwa Na Mwanzilishi wa chama cha mitindo Tanzania Mustafa Hassanali alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na chama hiko amesema chama hiko kimeanzishwa kuwa chenye nguvu na taaluma ya uwezo wa kukuza na kuimarisha sekta ya mitindo nchini  pia kuunga mkono juhudi za rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dkt.john pombe Magufuli katika kuifanya nchi yetu kuwa  katika uchumi wa kati wa Viwanda ifikapo mwaka 2025.

    Kwa upande wake Rais wa shirikisho la sanaa nchini Adrian Nyangamalla amewapongeza wabunifu kwa hatua nzuri  walioichukua kwani kimekuja wakati muafaka ambapo wasanii mbalimbali wanatakiwa kujisajili kwa makundi wawe wananufaika kupitia na wawe wanachangia uchumi wa nchi.

    Naye Katibu Mtendaji wa Basata  Godfrey Mngereza amesema hatua iliyofikiwa na wanamitindo itasaidia wasanii kuwa katika utawala bora hivyo ni jambo la kuungwa mkono na Basata itashirikiana hayo began kwa began kuhakikisha chama hiko kinapiga hatua zaidi.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI