• Breaking News

    ..

    ..

    Wednesday, 10 January 2018

    Watanzania wanatakiwa kuuthamini utalii wa ndani



    Na Apolonia Kisite
    Waziri wa maliasili na utali Khamisi Kigwangala amewataka watendaji wa wizara ya maliasili na utalii kushirikiana kwa pamoja ili kuhakikisha sekta ya utalii inakua nchini.
    Akizungumza jijini Dar es salaam katika hafla ya uzinduzi wa kamati ya kitaifa ya kuratibu shughuli za maandalizi za mwezi maalum wa maadhimisho ya urithi wa taifa la Tanzania amesema sekta ya uatalii imekuwa na mchango mkubwa  katika kuchangia pato la taifa kukua.
    Sambamba na hayo Mhe.Kigwangala amesema mpaka sasa sekta ya utalii imekuwa imejikita zaidi katika utalii wa wanyama pori ili kuwavutia watalii wanaongia nchini kwa wengi wao wanavutiwa zaidi kuangalia wanyama pori.
    Aidha ameitaka kamati hiyo inayoandaa maadhimisho hayo wahakikishe wanaandaa mpango maalum wa kuelimisha jamii juu ya mila na tamaduni zao za kitanzania na kutangaza lugha ya taifa (Kiswahili) nje ya nchi.
    Kwa upande wa Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema wao kama kamati wanakazi kubwa ya kutumia maadhimisho hayo kuweka mikakati ya kuongeza utalii wa ndani kwani bado watanzania wengi hawana utamaduni wa kutembelea mbuga zetu na vivutio vya ndani

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI