Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya Nishati ijiridhishe na
ubora wa vifaa vinavyotumiwa na wakandarasi katika miradi ya umeme.

Ametoa
kauli hiyo leo wakati akizungumza katika kikao cha maendeleo ya
usambazaji umeme kilichofanyika , Ofisini kwake, Dodoma ambapo ametaka
iwasimamie wakandarasi hao kwa ukaribu ili kuhakikisha thamani ya
miradi inayotekelezwa inalingana na kiasi cha fedha wanacholipwa
wakandarasi hao.
Waziri Mkuu amesema wakati huu ambao Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wakiendelea na miradi ya usambazaji umeme, na kuongeza kwamba ni vema wizara hiyo ikajiridhisha na ubora wa vifaa.
“Wasimamieni wakandarasi kikamilifu na kama hamjaridhishwa na kazi wanayofanya msisite kuwachukulia hatua, tunataka wananchi wapate umeme.” Majaliwa
Amesema Rais Dkt. John Magufuli amedhamiria kuona umeme unasambazwa kwenye vijiji vyote nchini kwa lengo la kuboresha maendeleo ya wananchi.
Waziri Mkuu amesisiza kwamba ni lazima wakandarasi waliopewa jukumu hilo wasimamiwe kikamilifu ili mradi hiyo iweze kuwa na ubora unaostahili.
Kwa upande wake Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amesema tayari wakandarasi wanaotekeleza mradi wa REA namba tatu wameshaanza kazi.
Amesema kwa wakandarasi ambao bado hawajaanza wamekubaliana kwamba wataanza wakati wowote na wa mwisho utaanza Machi 2, 2018 na kuongeza kwamba wizara yake itahakikisha miradi yote ya kusambaza umeme inasimamiwa kikamilifu na inakamilika kwa wakati na katika ubora unaostahili. CHANZO EATV
Waziri Mkuu amesema wakati huu ambao Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wakiendelea na miradi ya usambazaji umeme, na kuongeza kwamba ni vema wizara hiyo ikajiridhisha na ubora wa vifaa.
“Wasimamieni wakandarasi kikamilifu na kama hamjaridhishwa na kazi wanayofanya msisite kuwachukulia hatua, tunataka wananchi wapate umeme.” Majaliwa
Amesema Rais Dkt. John Magufuli amedhamiria kuona umeme unasambazwa kwenye vijiji vyote nchini kwa lengo la kuboresha maendeleo ya wananchi.
Waziri Mkuu amesisiza kwamba ni lazima wakandarasi waliopewa jukumu hilo wasimamiwe kikamilifu ili mradi hiyo iweze kuwa na ubora unaostahili.
Kwa upande wake Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amesema tayari wakandarasi wanaotekeleza mradi wa REA namba tatu wameshaanza kazi.
Amesema kwa wakandarasi ambao bado hawajaanza wamekubaliana kwamba wataanza wakati wowote na wa mwisho utaanza Machi 2, 2018 na kuongeza kwamba wizara yake itahakikisha miradi yote ya kusambaza umeme inasimamiwa kikamilifu na inakamilika kwa wakati na katika ubora unaostahili. CHANZO EATV
No comments:
Post a Comment