Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, ameitaka jamii pamoja
viongozi wa dini kushirikiana na Polisi ili kutokomeza makosa mbalimbali
katika jamii ikiwemo, mauaji yatokanayo na wivu wa mapenzi, ulevi,
ubakaji ili kuiweka nchi salama zaidi.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania, IGP Simon Sirro.
IGP
Sirro ameeleza hayo leo Jijini Dar es Salaam ambapo amesema kuwa
takwimu za sasa zinaonyesha matukio ya aina hiyo yamekithiri sana nchini
Tanzania jambo ambalo jamii inapaswa kubadilika ili kupunguza matukio
hayo.
"Kuna makosa ambayo watu lazima wabadilike na hili haliitaji Jeshi la Polisi maana mimi nasimamia Sheria lakini kuna viongozi wa dini wazungumzie hayo mambo. Muumini wako akija Kanisani au Msikiti na ukimwambia katazo la Mungu anaweza akabadilika", alisema IGP Sirro.
Kwa upande mwingine, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Sirro amesema kuna makosa ambayo viongozi wa dini wakishiriki kwa ukaribu zaidi inaweza kupunguza huku akiitaka jamii kubadilika kitabia ikiwemo kuachana na ulevi wa kupindukia.
"Kuna makosa ambayo watu lazima wabadilike na hili haliitaji Jeshi la Polisi maana mimi nasimamia Sheria lakini kuna viongozi wa dini wazungumzie hayo mambo. Muumini wako akija Kanisani au Msikiti na ukimwambia katazo la Mungu anaweza akabadilika", alisema IGP Sirro.
Kwa upande mwingine, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Sirro amesema kuna makosa ambayo viongozi wa dini wakishiriki kwa ukaribu zaidi inaweza kupunguza huku akiitaka jamii kubadilika kitabia ikiwemo kuachana na ulevi wa kupindukia.
No comments:
Post a Comment