Mashuhuda
wa ajali hiyo wameiambia EATV Saa1 kuwa, ajali hiyo imetokea katika
makutano ya barabara ya Kajenge na Rose Garden eneo la Sayansi ilipokuwa
akiongoza magari
Juma Husein ambaye ni mkazi wa Sinza amesema, ajali hiyo imesababishwa na gari aina Hucher maarufu kama Daladala kushindwa kufunga breki baada ya kusimamishwa na trafiki na kisha kuligonga gari dogo aina ya Subaru ambalo lilikuwa limeruhusiwa kuondoka na kusababisha ajali iliyopelekea trafiki huyo kugongwa na gari jingine.
Ajali hiyo imetajwa kuhusisha magari matatu, majeruhi akiwemo trafiki huyo walikimbizwa hosptali kwa matibabu zaidi, aidha Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa trafiki huyo alivunjika mkono.
Juma Husein ambaye ni mkazi wa Sinza amesema, ajali hiyo imesababishwa na gari aina Hucher maarufu kama Daladala kushindwa kufunga breki baada ya kusimamishwa na trafiki na kisha kuligonga gari dogo aina ya Subaru ambalo lilikuwa limeruhusiwa kuondoka na kusababisha ajali iliyopelekea trafiki huyo kugongwa na gari jingine.
Ajali hiyo imetajwa kuhusisha magari matatu, majeruhi akiwemo trafiki huyo walikimbizwa hosptali kwa matibabu zaidi, aidha Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa trafiki huyo alivunjika mkono.
No comments:
Post a Comment