• Breaking News

    ..

    ..

    Friday 23 March 2018

    PROF. LIPUMBA AZUNGUMZIA BAJETI YA SERIKALI

    wingu%2Bla%2BhabariNA NOEL RUKANUGA, DAR ES SALAAM.
    Serikali imetakiwa kupanga bajeti inayotekelezeka ili kufanikisha utekelezaji wa shughuli za kimaendeleo zinazokusudiwa.
    Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati akitoa maazimio ya kikao cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa, Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) Prof. Ibrahim Lipumba, amesema kuwa serikali inapaswa kupanga bajeti kulingana na matumizi halisi.
    Prof. Lipumba amesema kuwa kwa mujibu wa takwimu za Benki Kuu ya Tanzania katika kipindi cha miezi saba kunzia julai mwaka wa jana hadi januari mwaka huu, serikali ilipanga kutumia shilling trilioni 15.5 lakini matumizi halisi yanakadiriwa kuwa shilingi trilioni 10.7.
    Amesema kuwa matumizi hayo ni sawa na asilimia 69 ya bajeti hiyo ambayo utekelezaji wake unasuasua kwa katika kipindi hicho serikali ilitenga shilingi trilioni 7.4 kwa ajili ya kutumia kwenye miradi ya kimaendeleo.
    “Ni vema bajeti zetu zikawa zinazingatia hali halisi kutokana kumekuwa na matumizi madogo kuliko bajeti” amesema Prof. Lipumba.
    Prof. Lipumba ambaye ni mchumi anafafanua kuwu makadirio ya ukusanyaji wa kodi ni mkubwa kuliko ukusanyaji halisi kwani mwezi julai mwaka jana hadi januari mwaka huu mapato yote ya serikali yalikadiriwa kuwa shilingi trilioni 11.7 lakini makusanyo ni trilioni 10.2 ambapo sawa na asilimia 88.
    Amesema kumekuwa na mzunguko mdogo wa fedha (Currency in circulation) kutoka shilingi trlioni 3.8 kwa mwezi oktoba 2015 na kufikia shilingi trilioni 3.4 april mwaka wa jana, jambo ambalo sio rafiki kwa uchumi wa nchi.
    Hata hivyo mchumi huyo ameipongeza serikali kwa juhudi za kukusanya mapato na kutekeleza miradi mikubwa ikiwemo kujenga reli ya kisasa pamoja na kufua umeme wa maji kwenye maporomoko.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI