• Breaking News

    ..

    ..

    Wednesday 11 July 2018

    Mwenge wa Uhuru wazindua miradi ya sh.bilioni 3.7



    MWENGE wa Uhuru umehitimisha ziara yake Mkoani Dar es Salaam kwa kuzinda miradi tisa yenye thamani ya sh.bilioni 3.7 ,  wilayani Temeke.

    Mwenge uliingia moan Dar es Salaam, Julai 7 mwaka huu ukitokea Kusini Pemba, ambapo , katika Mkoa wa Dar es Salaam, jumla ya miradi 33 ilizinduliwa.

    Miradi iliyozinduliwa Wilayani Temeke ni  mardi wa usambazaji maji mtaa wa Mabatini, Tandika  wenye thamani ya sh. Milioni  253.6.

    Mradi mwingine  ambeo ulikaguliwa ni wa elimu ya mafunzo ya ufundi bila  malipo kwa vijana   wanaoishi katika mazingira hatarishi, Kata ya Temeke, wenye thamani ya sh.milioni  4.2.

    Pia  Mwenge wa Uhuru, uliweka jiwe la msingi katika mradi wa ukarabati  wa vyumba  vya madarasa 20, ofisi mbili, maabara tatu, stoo moja, choo kimoja chenye matundu  mawili katika Shule za Msingi na Sekondari   ya Muungano katika Kata ya Temeke, ambapo thamani yake ni sh.milioni 489.5.

    Mwenge wa Uhuru pia  uliweka jiwe la msingi  katika mradi wa  ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje  la ghorofa  mbili  katika Kituo cha Afya  Yombo Vituka, unaogharimu sh.bilioni 2.12.

    Pia, ulizindua mradi wa kilimo  cha kitalu  na nyumba ya kijani eneo la Yombo Vituka  unaogharimu sh.milioni 22.00

    Mwenge uliweka jiwe la musing katika mradi wa ujenzi wa daraja  kiwango cha karavati  la midomo mitatu  katika Mtaa wa Mashine ya Maji Kata ya Buza uliogharimu sh.milioni 685.9.

    Pia, mwenge  ulizindua  mrafi wa uboreshaji  wa mazingira na bustani  ya maua  kwa kikundi cha  vijana cha Kwetu Pazuri, pamoja na uzinduzi wa gari ya kuzolea taka  la Halmshauri ya Manispaa ya Temeke ambapo miradi hiyo imegharimu jumla ya sh.milioni 162.00

    Ziara hiyo ya mbio za Mwenhe wa Uhuru iliendelea kwa kuzindua na kukagua  klabu a  ya kupiga vita dawa  kulevya  na klauw  ya wapinga rush  ambapo  bio za mwenge zilihitimishwa  kwa  kukagua  mapambano  dhidi ya  malaria, ukimwi na Kazi  za kimono  za vijana  na anawake, Barbara ya Kilwa katika eneo la Mbagala Rangi Tatu.

    Akizungumza wakati wa uzinduzi wa miradi hiyo, Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Mwaka 2018, Mhandisi Charles Kabeho alipongeza viongozi wa hamashauri hiyo kwa kusimmia kikamilifu shughuli za  maendeleo.

    “Ninawapongeza kwa utekelezaji wa miradi hii.Serikali yetu ya awamu ya tano chini ya Rais Dk. John Magufuli inaitaji maendeleo kwa wananchi wake ambapo imeweka kipaumbele katika elimu, ujenzi wa miundo mbinu na afya.Temeke mmetekeleza,”alisema Mhandisi Kabeho.

    Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Felix Lyaniva, alisema, wamejidhatiti kuhakikisha miradi  muhimu inatekelezwa kwa wakati ili kuharakisha maendeleo.

    “Tunamiradi mingi inayoendelea na hai uliyozindua ni miongoni mua mirai michache tu tunayoitekeleza. Temeke tumejipanga kikailifu kuhakikisha  tunaendana na quasi ya serial ya away ya tank chini ya Rais Dk. Magufuli,”alisema Lyaniva.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI