• Breaking News

    ..

    ..

    Thursday, 3 November 2016

    TIGO YAJA NA VIFIRUSHI VIPYA VYA INTANETI ‘MEGA MIX’

     Ofisa mkuu wa Biashara wa Tigo Shavkat Berdiev (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu Kampuni ya Simu ya Tigo kuja na vifurushi vipya vya intaneti ;Mega Mix’. Kulia ni Meneja Chapa wa Tigo, William Mpinga.
     Meneja Chapa wa Tigo, William Mpinga (kulia), akizungumza katika mkutano huo.
    Mkutano na wanahabari ukiendelea.
     
    Kampuniinayoongoza kwa mtindo wa maisha ya kidijitali Tigo Tanzania leo imetangaza
    kuanzishwa kwa  ofa ya MEGA MIX ambayo itakuwa inatoa vifurushi vya
    intaneti ambayo vitawazawadia wateja dakika za ziada kwa ajili ya kupiga simu.
    Ofa  hii itawapatia wateja  urahisi wa kutumia vifurushi hivi
    vipya kupitia kifaa chochote kinachotumia intaneti  zikiwemo simu za
    mkononi  na modemu. 
     
    Akitangaza vifurushi vya
    Mega Mix kwa waandishi wa habari Dar es Salaam leo Ofisa mkuu wa Biashara wa Tigo Shavkat Berdiev
    alivielezea vifurushi hivyo  kama “hatua moja mbele ya mabadiliko katika
    soko  inayotoa   vifurushi sahihi zaidi: ikiwa ni suluhisho kwa
    watumiaji wote wa data ndani ya sekta ya mawasiliano ya simu nchini Tanzania.”
     
     Shavkat
    aliongeza, “Wateja wetu hivi sasa  wana uhuru wa kuchagua
    kutoka katika simu zao  kifurushi chochote wanachokitaka kikiwa na
    dakika za ziada  zitakazo wawezesha kuunganishwa na wapendwa wao
    wakati tunapoukaribisha msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka.”
     
     Aliendelea kusema,
    “Kwa vifurushi vipya wateja wanaweza kuhabarishwa kwa wakati katika mtiririko
    wa  kuunganishwa  na  wenzi wao na kuwa bega kwa bega na
    yanayotokea  sehemu mbalimbali duniani. Vifurushi hivi vipya vinaendelea
    kuonesha jinsi Tigo ilivyojikita katika kuboresha mabadiliko katika mtindo wa
    maisha ya kidijitali na inavyoongoza katika kutoa  teknolojia ya kisasa
    pamoja na ubunifu  kwa wateja wetu.
     
    “Wateja wetu vilevile
    wanaweza kuzipata taarifa za kidunia, kutafuta  kupitia Google, kusikiliza
    muziki, kuangalia video, kupakua na hata  kutiririsha sinema. Hii ni kwa
    sababu  tumeunda vifurushi hivi  kwa kuzingatia mahitaji ya kipekee
    ya wateja  wetu  kwa kufanya uwepo urahisi katika kuchagua
    kutoka  katika kifurushi kimoja  kwenda kingine kutegemeana na
    hali ya kifedha ya wateja.”
     
    Aidha Meneja Chapa wa
    Tigo, William Mpinga alisema, “Kutokana na teknolojia ya 4G LTE kupatikana
    kwa hivi sasa katika miji 20 vifurushi vya  Mega Mix
    kunafungua enzi mpya za kufikia intaneti kusiko na ushindani, ambako
    kutaondoa vikwazo  na kuwawezesha watumiaji  kuona mengi, kusikia
    zaidi na hatimaye  kupata yaliyo mazuri katika maisha.”
     
    Mpinga aliongeza, “Mteja
    anachotakiwa kukifanya ili kupata  vifurushi vya Mega Mix ni kupiga
    *148*00#  halafu chagua, ‘Vifurushi vya intaneti.”

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI