• Breaking News

    ..

    ..

    Wednesday, 15 November 2017

    ugonjwa wa kisukari unavyosababisha upofu wa macho.

    Na stahmili mohamed

    Ikiwa ni mwezi wa kisukari duniani, ugonjwa wa kisukari umeonekana kuwa kisababishi kikubwa cha ugonjwa wa upofu wa macho nchini Tanzania. 

    Hayo yamesemwa Leo na muuguzi wa international hing hospital catheline Chacha ambaye pia amebainisha ni kwa jinsi gani ugonjwa huo unapelekea mtu kupoteza uwezo wa kuona.

    Catheline amesema kuwa, ugonjwa wa kisukari Unasababisha mishipa ya macho kuharibika na kuvunjika jambo ambalo hupelekea damu kuvuja na kusababisha pazia la jicho kuhama kabisa kwenye sehemu yake hivyo mtu kupoteza uwezo wa kuona.
    "Kisukari inaharibu mishipa ya macho na kufanya mishipa kuvunjika jambo ambalo hupelekea damu kuvuja na kusababisha pazia la jicho kuhama kabisa kwenye sehemu yake" amesema catheline.

    Pia catheline ameongeza kuwa kisukari haiharibu mishipa ya macho peke yake bali husababisha vitu vingi sana kuharibika ndani ya macho.

    "Kisukari pia inaharibu vitu vingi sana kwenye macho na si mishipa tu" ameongeza Catherine
    Mwisho amewahasa watanzania kujenga mazoea ya kutembelea vituo vya afya Mara kwa Mara ili kujua maendeleo ya afya zao kwani ni bora kuwahi tatizo mapema kuliko kuchelewa.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI