• Breaking News

    ..

    ..

    Monday, 13 November 2017

    Wafanyakazi wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Watakiwa kuzingatia Kanuni na Sheria katika kutekeleza Majukumu

      Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi. Suzan Mlawi akizungumza na Watumishi wa Wizara hiyo waliopo katika kituo cha Dar es Salaam leo ambapo amewataka kufanya kazi kwa bidii na kufuata Sheria za Utumishi wa Umma.
    Na Anitha Jonas – WHUSM
    Dar es Salaam
    Katibu Mkuu Waziri wa Habari Utamaduni  Sanaa na Michezo Bi.Suzan Mlawi amewataka wafanyakazi wa Wizara hiyo kuzingatia Kanuni Sheria na Utaratibu kwa katika kufanya kazi.
    Bi. Mlawi ametoa wito huo  alipokuwa akifanya kikao na wafanyakazi wa wizara waliyoko jijini Dar es Salaam ikiwa ni mara yake ya kwanza kukutana na wafakazi hao baada kuapishwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli.
    “Ninawataka mfanye kazi kwa kushirikiana na upendo na kila mmoja awajibike katika nafasi yake na mhakikishe mnatoa huduma kwa wateja kwa wakati na upendo,”alisema Bibi Mlawi.
    Akiendelea kuzungumza katika kikao hicho Katibu Mkuu huyo alitoa angalizo kwa watu wanaopenda kungangania kazi na badae kushindwa kuzitekeleza  na kusisitiza suala la uwajibikaji ni kwa wote na kama mtu ameelemewa na kazi hana haja ya kungangania kazi ambayo anaona hataweza  kuitekeleza kwa wakati.
    Naye   Mwenyekiti wa TUGHE  Bi Magret Mtaki alisema wanyakazi wanaima kubwa na wewe kuwa utawasaidia kutatua changamoto zao ikiwemo ukosefu wa vitendea kazi   na mambo mbalimbali kama ilivyoelezwa na Mkurugenzi wa Michezo

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI