Wakurugenzi, meya na wenyeviti wa halmashauri zote saba Mkoani Singida wakiendela na katika kikao cha Jumuiya za
Serikali za mitaa Tanzania (ALAT).
Serikali za mitaa Tanzania (ALAT).
……………………………………………………………………………………….
Na Mwandishi Wetu Singida
Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhandisi Mathew J. Mtigumwe amewaasa
wakurugenzi, meya na wenyeviti wa halmashauri zote saba Mkoani Singida kutumia
vikao vya mafuzo ya Jumuiya za Serikali za mitaa (ALAT) kutatua kero za
halmashauri.
wakurugenzi, meya na wenyeviti wa halmashauri zote saba Mkoani Singida kutumia
vikao vya mafuzo ya Jumuiya za Serikali za mitaa (ALAT) kutatua kero za
halmashauri.
Mhandisi Mtigumwe ameyasema hayo wakati akifunga mafunzo ya ALAT
mkoa wa Singida na kuwasisitizia kuwa mafunzo hayo yawe na tija na sio kukaa
vikao visivyo na matokeo chanya.
mkoa wa Singida na kuwasisitizia kuwa mafunzo hayo yawe na tija na sio kukaa
vikao visivyo na matokeo chanya.
Ameongeza kuwa katika kipindi cha miezi sita tangu ateuliwe na
Mhe Rais amebaini halmashauri zina changamoto za ukusanyaji hafifu na
usioridhisha wa mapato ya ndani pamoja na mikataba mibovu inayosainiwa na
halmashauri na hivyo kuiletea hasara serikali.
Mhe Rais amebaini halmashauri zina changamoto za ukusanyaji hafifu na
usioridhisha wa mapato ya ndani pamoja na mikataba mibovu inayosainiwa na
halmashauri na hivyo kuiletea hasara serikali.
Mhandisi Mtigumwe amesema kumekuwa na migogoro ya ardhi
inayosababishwa na maafisa ardhi wasio kuwa waadilifu, watumishi na madiwani
kujimilikisha ardhi na vibanda kinyume na utaratibu pamoja na kutotengwa kwa
asilimia kumi ya mapato ya ndani kwa ajili ya wanawake na vijana.
inayosababishwa na maafisa ardhi wasio kuwa waadilifu, watumishi na madiwani
kujimilikisha ardhi na vibanda kinyume na utaratibu pamoja na kutotengwa kwa
asilimia kumi ya mapato ya ndani kwa ajili ya wanawake na vijana.
“Halmashauri hazijatenga maeneo ya viwanda vidogo na vya kati,
uchafu umekithiri katika maeneo mengi, watumishi wanaokiuka taratibu
hawachukuliwi hatua za kinidhamu na mawasiliano hafifu kati ya viongozi na
watumishi, viongozi na viongozi na hata watumishi wenyewe, hizi ni baadhi ya
changamoto ambazo kikao cha ALAT kitumike kuzitafutia majibu, alisisitiza.
uchafu umekithiri katika maeneo mengi, watumishi wanaokiuka taratibu
hawachukuliwi hatua za kinidhamu na mawasiliano hafifu kati ya viongozi na
watumishi, viongozi na viongozi na hata watumishi wenyewe, hizi ni baadhi ya
changamoto ambazo kikao cha ALAT kitumike kuzitafutia majibu, alisisitiza.
Mhandisi Mtigumwe amewasisitiza wakurugenzi kuunda mabaraza ya
wafanyakazi na halmashauri zenye mabaraza hayo basi vikao vifanyike ili kero na
changamoto za watumishi zisikilizwe na kutafutiwa ufumbuzi.
wafanyakazi na halmashauri zenye mabaraza hayo basi vikao vifanyike ili kero na
changamoto za watumishi zisikilizwe na kutafutiwa ufumbuzi.
Kwa upande wao meya, wenyeviti na wakurugenzi wa halmashauri
wamemshukuru mkuu wa Mkoa kwa nasaha alizowapa na kuahidi kuyatumia mafunzo ya
ALAT katika kuleta mabadiliko katika halmashauri zao.
wamemshukuru mkuu wa Mkoa kwa nasaha alizowapa na kuahidi kuyatumia mafunzo ya
ALAT katika kuleta mabadiliko katika halmashauri zao.
Wajumbe walipata fursa ya kujifunza juu ya Mfumo ya serikali za
mitaa Tanzania bara, ukusanyaji wa mapato ya ndani kwenye halmashauri,
utaratibu wa manunuzi katika serikali za mitaa , uwazi na uwajibikaji na
mawasiliano kwa viongozi.
mitaa Tanzania bara, ukusanyaji wa mapato ya ndani kwenye halmashauri,
utaratibu wa manunuzi katika serikali za mitaa , uwazi na uwajibikaji na
mawasiliano kwa viongozi.
No comments:
Post a Comment