SHULE ya Sekondari ya Mtakuja iliyopo Kunduchi inakabiliwa na uhaba wa Mwalimu wa Hesabu, hali iliyosababisha, Diwani wa Kata hiyo Michael Urio kumlipa mshahara mwalimu wa somo hilo.
''Nilivyoona kuna uhitaji wa mwalimu wa hesabu kidato cha kwanza na cha pili, niliamua kumtafuta mwalimu ambaye nitamlipa mshahara ili aweze kuwasaidia watoto hao'', alisema.
Aidha Diwani huyo alisema wanafunzi hao wamekuwa katika mazingira kama hayo, tangu mwezi februali mwaka huu mpaka sasa, wala hakuna dalili za kupatikana mwalimu wa Serikali.
Hapa alikuwa katika ziara ya kutembelea na kusikiliza kero za wananchi na kutatua matatizo yanayowakabili.
mwisho
No comments:
Post a Comment