Balozi wa Kuwait Jasem Al-Najem ametoa msaada wa vifaa mbambali katika hospitali ya Taifa Muhimbili.
Msaa huo umehusisha mashine tano za kupimia presha,dawa za kutibu magonjwa mbali mbali.
Akizungumza katika makabidhiano wa vifaa hivyo Balozi huyo ameahidi kutoa misaada mbalimbali katika hospitali ya Muhimbili ikiwemo msaada wa vifaa kwaajili ya upasuaji wa moyo, kutoa vifaa vitakavyo saidia kuhifadhi damu.
Kwa upande wa mwakilishi kutoka wizara profesa Ayubu Magimba amesema wamekubaliana na Balozi wa Kuwait kuweka kituo cha kuhifadhi damu katika taasi ya Jakaya kikwete ilikupunguza tatizo la damu.
" watatuwezesha Jakaya kikwete tuwe na kituo cha kuhifadhi damu na watatuwezesha kufanya kampeni ya uchangiaji damu nchini ambayo itafanyika kabla ya mwezi ujao.hayo amesema Magimba.
Balozi wa kuwait akikabidhi vifaa vya matibabu katika tasisi ya tiba mifupa na mishipa ya fahamu (MOI)
Balozi wa kuwait akikabidhi vifaa vya matibabu katika tasisi ya Tasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete
Balozi wa kuwait akikabidhi vifaa vya matibabu katika tasisi ya Tasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete
No comments:
Post a Comment