• Breaking News

    ..

    ..

    Wednesday, 23 November 2016

    MAKONDA ALIA NA WAFANYA BASHAR WA SOKO LA SAMAKI



    MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda, amepiga marufuku  wauzaji holela wa samaki na mbogamboga mitaani na kuagiza  jeshi la polisi na halmshari zote mkoani humo kuwakamata wafanyabishara watakao kikuka agizo hilo.
    Makonda ametangaza hatua hiyo , jana, wakati alipotembelea Soko la Kimataifa la Samaki (Feri) na kuzungumza na wafanyabiashara katika soko hilo ambao walieleza kuwa, moja ya changamoto zinazo wakabili ni pamoja na kuzagaa kwa wafanyabiashara  huria wa samaki hususan katika vituo vya mabasi ya daladala na bararani mkoani humo.
    Wafanyabiashara hao, walidai kuwa, hali hiyo inahatarisha  uhai wa soko hilo kwani watu wengi hawafiki kununua samaki  katika soko hulo,  badala yake huishia kununua  katika vituo vya mabasi  na mitaani.
    Mfanyabiashara Said Ally ‘Ngasa’ alimueleza  mkuu huyo waa mkoa kuwa, masoko  huria ya mitaani  yanasendelea kushamiri huku  viongozi wa halmshauri  na wananchi wakikaa kimya.
    “Hivi sasa kila kona kuna watu wanauza samaki  hasa katika vituo vya mabasi. Hapa feri tunakosa wateja. Wanaishia hukohuko mtaani. Hili soko litakufa kwa sababu watu hawaji tena tofauti na awali,”alisema Ngasa.
    Aliongeza;“Naomba wafanyabishara katika vituo vya mabasi washughulikiwe. Hapa soko linakufa. Biashara imepotea,”
    Mohamed Nasoro ambaye ni muuzaji wa mbogamboga katika soko hilo, alisema uuzwajji holela wa mbogamboga mitaani  unaua  soko la bidhaa hiyo, hivyo kumuomba mkuu huyo wa mkoa kuchukua hatua  dhidi ya wafanyabiashara waliozagaa mitaani.
    Mbali na  hayo  wafanyabiashara hao waliomba  kuboreshwa kwa miundombinu ya soko hilo ambayo imechakaa licha ya soko kuwa la kimtaifa.
    Kufuatia kilio hicho, Makonda alichua uamuzi  wa kupiga marufuku biashara ya samaki  na mbogamboga mitaani na kumuagiza Kamanda wa Operesheni , Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lucas Mkondya kuwashughulikia wafanyabiashara wote watakao kiuka agizo hilo kuanzia leo.

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI