• Breaking News

    ..

    ..

    Friday, 11 November 2016

    MKURUGENZI wa kampuni ya Star Natural Products amewataka watanzania kumuunga mkono Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli


    MKURUGENZI na Mbunifu wa kampuni ya Star Natural Products  George Buchafwe amewataka watanzania kumuunga mkono Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli katika kutekeleza kauli yake ya Tanzania viwanda pamoja na kuwa wabunifu,wazalishaji na kulipa kodi
    Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es salaam jana wakati maonyesho ya kibiashara yaliyofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee alisema kuwa nchi yoyote haiwezi kuendelea pasipo kuwekeza katika viwanda vidogo vidogo.

    Alisema kuwa kampuni yake imewekeza katika kutengeneza sabuni na mafuta yaliyotengenezwa na mawese na imeajiri watu Zaidi ya 25, na kuwashauri vijana wasikae mtaani kusubiri kuajiliwa badala yake wajishughulishe.

    Aliongeza kuwa kiwanda chake kipo chini ya SIDO na kina dhamana pana ya kukuza viwanda vidogo,kutoa mafunzo na kuendeleza mawazo kwa wajasiliamali wapya wanaotaka kujiunga na uzalishaji wa kuchakata mafuta ya mawese na uzalishaji wa sabuni bora.

    “Katika uzalishaji tumebuni mashine nzuri kwa ajili ya uzalishaji wa mafuta na sabuni katika kuzingatia lengo kuu la millennia ya kupiga vita umaskini, na kuumunga mkono Rais Magufuli na nchi yoyote haiwezi kuendeloea pasipo watu wake kujishughulisha”. Alisema George

    Kwa upande wake Mhasibu Mkuu wa Mic Global Risks Scholastica Mtey alisema kuwa lengo la maonyesho hayo ni kutoa fursa kwa watanzania kujifunza kuwa kampuni yake inatoa bima ya afya inayowezesha kutibiwa nchi aipendayo


    Alisema kuwa mtu akijiunga na huduma hiyo anapata uhuru wa kuchagua nchi au Taifa alitakalo na kampuni hiyo itasimamia huduma zote za matibabu , nauli na gharama zote atakazozitumia na kuwataka watanzania kujiunga kwa wingi na mfuko huo

    No comments:

    Post a Comment

    HABARI

    HABARI

    MICHEZO

    LOGO

    LOGO

    MAOJIANO

    BURUDANI